JK AWATAKA WANASAYANSI WA DUNIA KUTAFUTA SULUISHO LA NYAYO ZA LAETOLI

September 13, 2015

188 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikiwete akiweka jiwe la msingi katika jengo la kitega uchumi linalomilikiwa na Mamlaka ya hifadhi ya Bonde la Ngorongoro lililopo mjini Arusha.
………………………………………………
Na Mahmoud Ahmad,Arusha
Raisi Jakaya Kikwete amewataka wanasayansi wa dunia kutafuta suluhisho la nyayo za Laetoli kwani ni ufumbuzi pekee utakosaidia kuweka kumbukumbu sahihi ya mwanadam wa kale na si kufukia eneo hilo bali kuliendeleza ndio jawabu la msingi kwa kuwa hawajashindwa kufanya utafiti juu ya eneo hilo.
Kauli hiyo  aliitoa wakati akiweka jiwe la msingi la jengo la jakaya kikwete ngorongoro tower lililopo katikati ya jija la arusha litakalo kuwa kichocheo cha uchumi linalomilikiwa na mamlaka ya hifadhi za ngorongoro.
Raisi alisema kuwa ili uhifadhi wa mwanadam wa kale uendelee kuweza kuipatia mamlaka mapato lazimaWabuni njia ya kutolitegemea shimo la kreta pekee na waangalie namna watalii watangalia wanyama wakiwa nje ya shimo la kreta kwani shimo hilo pekee ni kivutio na bila kusahau historia ya mwanadam wa kale.
 Pia aliwataka kuangali suala la kuwapa changamoto wanasayansi wa dunia ni jinsi gani ya kuhifadhi nyayo za Laetoli zitakazosaidia kuweka sawa histori ya mahali hapo na ya mwanadam kwa eneo hilo ni urithi wa dunia na kila mkazi wa eneo hilo anatakiwa kujivunia na kutunza uhifadhi wake kwa historia ya baadae.
Aidha aliitaka mamlaka ya hifadhi za ngorongoro kuangalia ni namna gani wataweza kuisaidia jamii ya eneo hilo kufanya maisha mengine bila ya kutegemea kilimo kwani jicho la ulimwengu linaangalia eneo hilo kama eneo la urithi wa dunia unaosaidia uhifadhi.
“Ongezeni maeneo ya vivutio katika hifadhi yenu kama mgeni kuangalia wanyama akiwa nje ya kreta hii itasaidia kuvuta watalii wengi watakao kuja kutembelea hifadhi na kuongeza mapato”alisema Dk kikwete
Alisema kuwa pamoja na kuangalia eneo hilo alimuagiza mkurugenzi wa mambo ya kale kukaa na wanasayansi wa dunia kulipatia majawabu suala la laitolya kwani ufumbuzi wa kufukia eneo hilo si jawabu sahihi la kutunza historia ya eneo hilo.
Awali akimkaribisha Mh.Raisi, Naibu waziri wa maliasili na utalii Mahmoud mgimwa alisema kuwa jengo hilo ni adhma ya mda mrefu ya mamlaka hiyo kuwa na kipato nje ya biashara ya utalii na kuwa jengo hilo limepewa jina la jk ngorongoro tower kwa kujua kuwa yeye ni Raisi ni mhamasishaji wa utalii kwa kuutangaza duniani kote alipotembelea
Alibainisha kuwa usanifu wa jengo hilo umeangalia wanyama kwani mbele na juu kuna pua ya tembo na juu pembe za nyati ikiwa ni ishara ya kutangaza utalii na kuipatia mamlaka hiyo mapato nje ya biashara ya utalii.
Naye  mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mamlaka balozi Mwanaid maajar alisema kuwa 
 jengo hilo litakalo kuwa na ghorofa15 litakapokamilika litagharim bilioni 42 za kitanzania na linajengwa na kampuni ya kichina ya Catic International Engineering na kuweza kutoa ajira kwa wakazi wa jiji la arusha na ni kichocheo cha maendeleo kwa wakazi hao.alisema kuwa jengo hilo linatarajiwa kukamilika mwakani mwezi november nalitasaidia kuongeza mapato mamlaka hiyo na kuwa wazo hilo lilibuniwa na bodi iliyopita mwaka 2010 na ujenzi wake kuanza miezi miwili iliyopita na hadi sasa ujenzi upo ghorofa ya tatu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »