NA MASANJA MABULA,PEMBA.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kuwa ujenzi wa minara ya majaribio ya umeme wa kutumia upepo na jua ni hatua za kukabiliana na tatizo la kukatika katika kwa nishati ya umeme visiwani humo .
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kuwa ujenzi wa minara ya majaribio ya umeme wa kutumia upepo na jua ni hatua za kukabiliana na tatizo la kukatika katika kwa nishati ya umeme visiwani humo .
Makamo
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amesema kuwa kukamilika
kwa ujenzi wa minara hiyo kutaondoa tatizo la kukatika katika umeme .
Kauli
hiyo ameitoa wakati alipotembelea ujenzi wa mnara wa umeme wa kutumia
upepo na jua katika shehia ya Kiuyu Mbuyuni Wilaya ya Micheweni Mkoa wa
Kaskazini Pemba unaojengwa kwa ushirikiano kati ya SMZ na Jumuiya ya
Nchi ya Ulaya (EU).
Amesema
kuwa mradi huo pia utapunguza gharama za kulipia huduma hiyo na
kuongeza kwamba wananchi wengi watamudu kutumia huduma hiyo na hivyo
kukuza uchumi na kuongeza kipato cha familia zao .
Aidha
Seif ametumia fursa hiyo kuiwataka wananchi wa shehia hiyo kushirikiana
na watendaji wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ili kufanikisha ujenzi
wa mnara huo .
Makamo
wa pili wa Rais amewataka wananchi kuwa wastahamilivu na kuacha utafiti
ufanyike ili kubaini ni aina gani ya umeme unafaa na ambao hautaathiri
mazingira .
Akitoa
maelezo ya ujenzi wa mnara huo kwa Makamo Meneja Mradi Maulid Shirazi
Hassan amesema kuwa Jumla ya minara mitano ya umeme wa Upepo na Jua
inajengwa Unguja na Pemba.
Amesema kuwa Jumuiya ya Umoja wa Nchi za Ulaya (EU) imetoa jumla ya Uero milioni tatu kwa ajili ya kazi za awali za ujenzi wa minara mitano Unguja na Pemba .
Mradi
huo unajengwa kwa majaribio katika maeneo ya wazi kwa ajili ya
kufanyiwa uchunguzi utachukua miezi kumi na nane ambayo ni sawa na
mwaka mmoja na baada ya hapo ripoti ya wataalamu kuwasilishwa serikalini
.