KIUNGO wa Timu ya Coastal Union,
Godfrey Wambura amesema kuwa tuzo ya uchezaji bora ya mwezi wa February
aliyoipata imempa mzuka wa kuhakikisha anajipanga imara ili kuendelea kufanya
vizuri.
Wambura ambaye alijiunga na Coastal
Union katika drisha dogo akitokea klabu ya Kagera Sugar alisema hayo juzi mara
baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo pamoja na hundi ya sh.milioni moja kutoka kwa
wadhamini wa Ligi hiyo Vodacom.
Akizungumza jana, Wambura alisema
kuwa anaamini uteuzi huo wa uchezaji bora uliofanywa na bodi ya Ligi kuu
ulikuwa makini na ndio maana umeweza kumuwezesha kupata nafasi hiyo ambayo
alikuwa akiiwaza kwa kipindi cha muda mrefu.
“Tuzo hii imenipa hamasa ya kuhakikisha ninatumia vizuri nafasi yangu
kama mchezaji lengo likiwa kuipa mafanikio timu yangu hasa katika harakati za
kucheza ligi kuu kwa ufanisi mkubwa “Alisema Wambura.
Hata hivyo aliwataka wachezaji wengi
kujituma na kucheza mechi kwa juhudi kubwa ili kuweza kupata nafasi za
kuwawezesha kuonekana na kuchaguliwa kuwa wachezaji bora kama ilivyokuwa kwake.