WAKUU WA TAASISI ZA KUZUIA RUSHWA BARANI AFRICA WAKUTANA ARUSHA KUANGALIA JINSI WATAWEZA KUPAMBANA NA KUFIKIA MALENGO YA KUTOKOMEZA RUSHWA NDANI YA BARA LA AFRICA

May 11, 2015

SAM_2509
Mwenyekiti wa bodi ya ushauri ya kupambana na maswala ya rushwa katika umoja wa Africa kutoka Ghana Mh.Daniel Batidam akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari jijini Arusha  katika ukumbi wa mikutano AICC katika kuangalia jinsi gani wataweza kupambana na kufikia malengo ya kutokomeza Rushwa ndani ya Bara La Africa.(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_2498
Makamu Mwenyekiti bodi ya ushauri ya kupambana na maswala ya rushwa katika umoja wa Africa Mh.Florince Ziyambi kutoka Zimbabwe
SAM_2494
Muongoza vikao kutoka Kenya Mh.John Tuta akitambulisha wajumbe
SAM_2497
SAM_2499SAM_2503
SAM_2514
Mwaandishi wa habari Merry Mwita akiuliza maswali katika mkutano huo
SAM_2504
Muonekano ndani ya ukumbi
SAM_2506
SAM_2522
Picha ya Pamoja
Wakuu wa taasisi za kuzuia Ruswa barani Africa wamekutana  katika ukumbi wa mikutano AICC katika kuangalia jinsi gani wataweza kupambana na kufikia malengo ya kutokomeza Rushwa ndani ya Bara La Africa.
Wakuu hao ambao ni wajumbe wa Bodi ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa barani Afrika AUABC iliyopo chini ya jumuia ya muungano wa nchi za Afrika ambapo mwenyekiti wa Taasisi ya AUABC Jaji Daniel Batidam amesema kuwa wanatarajia kwa mkutano huu utasaidi kupunguza makali ya Ruswa ndani ya bara hili.
Amesema kuwa kiwango kikubwa wanaangalia jinsi gani wataweza kuondoa ruswa katika taasisi za jamii kwa maana ndio zinazochangia kwa kiasi kikubwa maenbdeleo ya nchi zetu za kiafrika.
Pamoja na hayo amesema kuwa tatizo kubwa la Rushwa ndani ya bara la Afrika ni mfumo uliopo ambao unakuwa unaweka mianya ya rushwa pamoja na hayo alisisistiza kwa wananchi kuacha kutoa rushwa ili kuiondoa kabisa.
Bodi hiyo imeundwa na watu 11 kutoka nchi mbalimbali barani Africa

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »