RC MKOA KASKAZINI PEMBA:ASEMA NI JUKUMU LA VIONGOZI WA SIASA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUTATUA KERO

May 19, 2015
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini PEMBA Mhe Omar Khamis Othman amesema ni jukumu la viongozi wa siasa kushirikiana na serikali kutatua kero zinazowakabili wananchi katika maeneo yao .

Amesema kuwa viongozi wa majimbo wanashindwa kutambua wajibu na majukumu yao hali ambayo inapelekea wananchi kukabiliwa na changamoto ambazo zinaweza kutatulia na viongozi hao .

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mabandani Shehia ya Ukunjwi Wilaya ya Wete waliofika Ofisini kwake  kulalamikia ubovu  wa barabara , amesema kuwa viongozi wa majimbo wanao uwezo mkubwa kulipatia ufumbuzi .

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi wa Kijiji hicho kuendelea kuwa wastahamilivu wakati Serikali ya Mkoa akifanya juhudi za kuwasiliana na watendaji kutoka Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano ili waweze kuifanya matengenzo barabara hiyo na kufanya iweze kupitika .

Kwa upande wao wananchi wa Kijiji hicho amesema kuwa kutokana na ubovu wa barabara hiyo kunasababisha baadhi ya akinamama wajawazito kujifungulia njiani wakati wakipelekwa kwenye Kituo cha Afya na Hospitali .

Wamesema kuwa licha ya kero hiyo kuifikisha kwa Vingozi wao wa Jimbo , lakini badom ufumbuzi wake haujapatikana .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »