KITANDULA ATAKA WALIMU KUONGEZA BIDII DARASANI

May 08, 2015


NA SALUM MOHAMED,MKINGA.
 
MBUNGE wa jimbo la Mkinga, Dustun Kitandula, amewataka walimu shule za msingi na sekondari Wilayani hapa kuzidisha bidii ya ufundishaji darasani lengo likiwa ni kufuta alama ziro.

Akizungumza katika wiki ya Elimu iliyoadhimishwa Kiwilaya Wilayani humo jana, Kitandula alisema jitihada zaidi za walimu zinahitajika ili kuziwezesha shule zao kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa.

Alisema kipindi cha miaka ya nyuma shule za Mkinga zilikuwa zikishika nafasi za mwisho kimkoa na kitaifa na hivyo sasa walimu  kuonyesha bidii zao darasani ikiwa na panmoja na kuwa na mahusiano mazuri za wazazi wa wanafunzi.

“Tunatambua kuwa walimu wako na changamoto nyingi shuleni na nje ya shule----changamoto hii iwe chachu ya kufaulisha wanafunzi  na kufuta alama  ziro” Alisema Kitandula

Alisema Wilaya ya Mkinga mbali ya kuwa changa katika sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu lakini inaweza kupiga hatua mbele katika maendeleo kwa kuwandaa vijana katika elimu ili kuweza kuinua maendeleo ya Mkinga baadae.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Afisa elimu Sekondari Wilaya ya Mkinga, Omary Kombo, aliwataka wazazi na walimu kuhakikisha ujenzi wa maabara unakamilka kama ulivyopangwa.

Alisema kuwepo kwa maabara kila shule kutasaidia wanafunzi kusoma kwa vitendo pamoja na kufanya vizuri katika masomo yao ya sayansi na kuondosha uhaba wa walimu wa somo hilo.

Alisema Wilaya ya Mkinga iko na uhaba wa walimu wa somo la sayansi jambo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa kufanya vibaya katika mitihani yao ya Taifa.

“Wilaya ya Mkinga iko na uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi----nawaomba wanafunzi muliopo hapa jikiteni katika somo hili ili kuja kuwasaidieni ndugu zenu hapo baadae” alisema Kombo na kuongeza

“ Nanyi wazazi tushikamane kuwabidiisha vijana wetu kukosa masomo shuelni kwani huko nje kuna vishawishi vingi kama uvuaji wa samaki katika bahari yetu tunayopakana nayo” alisema

Aliwataka walimu kuwa na ushirikiano na wazazi pamoja na kamati zao ili kuweza kuleta maendeleo ya wanafunzi pamoja na mazingira ya shule na kumaliza majengo ya maabara.

                             


Mwanafunzi wa shule ya Sekondari  ya Gombero Wilayani Mkinga MkoanI Tanga, Mwabai Heri, akionyesha utaalamu wa kuchanganya kemikali za maabara wakati wa sherehe za  wiki ya Elimu Wilayani Mkinga leo asubuhi.


Mwanafunzi wa shule ya Sekindari ya Mapatano Wilayani Mkinga Mkoani Tanga, Haruni Justics, akionyesha utaalamu wa kuchanganya kemikali za maabara wakati wa sherehe za wiki ya Elimu Wilayani Mkinga juzi asubuhi.



Wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari Wilayani Mkinga Mkoani Tanga, wakisherehekea wiki ya elimu iliyofanyika kiwilaya Wilayani humo leo asubuhi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »