Mkuu
wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Rukia
Mtingwa (kushoto) akiwaongoza baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo katika
tukio la kujitolea damu lililoandaliwa na benki hiyo kuadhimisha Siku
ya Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam jana.
Meneja
Mahusiano ya Kibiashara wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Lukemelelo
Kaduma (katikati) akijitolea damu ikiwa ni sehemu ya matukio ya
wafanyakazi wa NBC kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani jijini Dar es
Salaam mwishoni jana. Anayemtoa ni mtaalamu wa damu kutoka Mpango wa
Taifa wa Damu Salama (NBTS), Peter Chami na kushoto ni mkazi wa Jiji la
Dar es Salaam, Benard Elikana.
Mmoja
wa wafanyakazi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Jolanda Songoro
(kushoto) akijitolea damu ikiwa ni sehemu ya matukio ya wafanyakazi wa
NBC kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam mwishoni
jana. Anayemtoa ni mtaalamu wa damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu
Salama (NBTS), Peter Chami.
Meneja
wa Idara ya Mikopo Midogo wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Jacob
Samuel (kulia) akijitolea damu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake
ikiwa ni sehemu ya matukio ya wafanyakazi wa NBC kuadhimisha Siku ya
Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam jana. Anayemtoa ni mtaalamu wa
damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS), Peter Chami.
Mmoja
wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, William Tendwa naye akishiriki tukio
lililoandaliwa na benki hiyo la kujitolea damu kuadhimisha Siku ya
Wanawake Duniani.
Baadhi
ya wafanyakazi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC wakijitolea damu
ikiwa ni sehemu ya matukio ya wafanyakazi hao kuadhimisha Siku ya
Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam jana. Anayewatoa damu kushoto ni
mtaalamu wa damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS), Peter
Chami.
Mkazi
wa Jiji la Dar es Salaam, Bernard Elikana akiungana na baadjhi ya
wafanyakazi wa NBC kujitolea damu kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani.
Kulia ni Petert Chami wa Damu Salama.
Mkazi
wa Mwananyamala Dar es Salaam Subira Omar akijitolea damu katika tukio
lililoandaliwa na Benki ya NBC kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani
jana. Anayemtoa ni Peter Chami kutoka Damu Salama (NBTS).
Mmoja
wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, John Nyaindi naye akishiriki tukio
lililoandaliwa na benki hiyo la kujitolea damu kuadhimisha Siku ya
Wanawake Duniani. Kushoto ni Daudi Mkawa kutoka Mpango wa Taifa wa Damu
Salama.
Mtaalamu
wa damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Peter Chami (kulia)
akimuandaa mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, Georgia Mwita ili aweze
kumtoa damu katika tukio hilo jijini Dar es Salaam jana.