Waziri
nchi Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI,Mh. Hawa Ghasia akizungumza mapema
leo katika siku ya kwanza ya mafunzo ya Wakuu wa Wilaya wapya ishirini
na saba yanayoendelea katika ukumbi wa hoteli ya St. Gaspar mjini
Dodoma. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa ambaye pia ni Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mh. Aggrey
Mwanri, Katibu Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne A. Sagini na Naibu Katibu Mkuu
TAMISEMI (Elimu) Bw. Zuberi Samataba.
Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne A. Sagini akitoa mada
kuhusu kazi na majukumu ya Wakuu wa Wilaya katika semina hiyo iliyoanza
leo tarehe 16 hadi 19 Machi 2015.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa UONGOZI Institute Profesa Joseph Semboja, ambaye pia
ndiye mwezeshaji mkuu wa mafunzo hayo akizungumza wakati wa mafunzo hayo
yanayoendelea mjini Dodoma. UONGOZI Institute ni taasisi iliyo chini ya
Ofisi ya Rais inayoshughulikia mafunzo kwa viongozi waandamizi
serikalini pamoja na kufanya utafiti na ushauri wa sera kwa serikali.
Mshiriki
wa mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mh. Shaban Kissu akichangia
mada wakati wa mafunzo. Mada moja wapo zilizojadiliwa leo ni kuhusu
mahusiano na mawasiliano baina ya serikali kuu na mamlaka za serikali za
mitaa.
Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni Mheshimiwa Paul Makonda akizungumzia kuhusu
changamoto mbali mbali za Wakuu wa Wilaya. Masuala yaliyojadiliwa ni
pamoja na maadili na sheria za kazi.
Baadhi
ya wahudhuriaji wa kundi la Wakuu wa Wilaya wapya ishirini na saba
wakifuatilia kwa makini mtoa mada (hayupo pichani) katika mafunzo ya
Wakuu wa Wilaya Wapya yanayoendelea mjini Dodoma.