Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la
Mwanga na Waziri wa Maji Mh. Prof. Jumanne Maghembe mara baada ya
kuwasili katika kata ya Kileo jimbo la Mwanga mkoani Kilimanjaro wakati
alipoanza ziara ya kikazi ya jimboni humo akikagua na kuhimiza ilani ya
uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali, Katika ziara
hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi
Taifa CCM.
Akizungumzia
tatizo la maji nchini kwa ujumla Prof. Maghembe amesema serikali iko
katika utekelezaji wa miradi ya maji awamu ya pili ambapo serikali
inatekeleza miradi ya maji katika miji mikuu mbalimbali hapa nchini,
ambapo ifikapo mwaka 2025 upatikanaji wa maji katika miji mbalimbali
kufikia asilimia 75% wakati katika jiji la Dar es salaam upatikanaji wa
maji utafikia asilimia 95, hata hivyo Prof. Maghembe amongeza kwamba
miradi hiyo inatekelezwa kwa gharama kubwa na serikali ina nia ya dhati
ya kumaliza tatizo hilo nchini kwa kiwango kikubwa. (PICHA NA KIKOSIKAZI
CHA FULLSHANGWE-MWANGA KILIMANJARO)
Mbunge wa jimbo la Mwanga na Waziri wa Maji Mh. Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na wananchi katika kata ya Kileo ambapo alikagua ujenzi wa nyumba za walimu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti wa kumbukumbu katika shule ya sekondari ya Kileo wilayani Mwanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Waziri Prof. Jumanne Maghembe wakikagua skimu ya umwagiliaji kijiji cha Kivulini wilayani Mwanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Waziri Prof. Jumanne Maghembe wakishiriki ujenzi wa mifereji ya skimu ya umwagiliaji kijiji cha Kivulini wilayani Mwanga.
Wananchi
wa Kijiji cha Kivulini wakitafakari jinsi ya kukwamua pikipiki yao
ambayo ilikwama kwenye moja ya mifereji yenye tope katika skimu hiyo ya
umwagiliaji.
Nape Nnauye akijaribu kuendesha Skaveta mtambo wa kuvunia mpunga katika kijiji cha Kivulini wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Nape Nnauye akishuka kwenye Skaveta mtambo wa kuvunia mpunga katika kijiji cha Kivulini wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Baadhi
ya wananchi waliojitokeza kumpokea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana wakati akiwasili katika kijiji cha Mangara Lembeni
wilayani Mwanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
na Waziri Prof. Jumanne Maghembe kushoto wakipiga makofi kuashiria
uwekaji wa jiwe la msingi katika ofisi ya CCM tawi la Mangara Lembeni wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Waziri Prof. Jumanne Maghembe akicheza ngoma ya asili ya wapare huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia ngoma hiyo wakati alipowasili katika moja na vijiji alivyotembelea na kuzungumza na wananchi wilayani Mwanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Waziri Prof. Jumanne Maghembe wakishiriki ujenzi wa jengo la KKKT Mwaniko wilayani Mwanga
Waziri
wa maji na Mbunge wa jimbo la Mwanga Prof. Jumanne Maghembe
akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mwaniko Ugweno wilayani
Mwanga
N
ape Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara kijiji cha Mwaniko Ugweno wilayani Mwanga.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi katika
mkutano huo uliofanyika kijiji cha Mwaniko Ugweno wilayani Mwanga
mkoani Kilimanjaro.
EmoticonEmoticon