Polisi Tanga yamkamata Mtuhumiwa mmoja aliyehusika kuwapora silaha Askari akiwa na silaha yenye risasi 29.

March 28, 2015

JESHI la Polisi Mkoani Tanga limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye alihusika katika tukio la uporaji wa silaha askari eneo la barabara ya nne na tano mtaa wa makoko jijini Tanga Januari 26 mwaka huu akiwa na bunduki yenye risasi 29.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Juma Ndaki alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Machi 18 mwaka huu eneo la Kabuku wilayani saa mbili usiku.
Ndaki alisema kuwa jinsi ya kukamatwa mtuhumiwa huyo ni baada ya jeshi hilo kupata taarifa za siri kutoka kwa wasamaria wema kuwa mtuhumiwa huyo alihusika katika unyang’anyi kwa kutumia silaha katika tukio ambalo lilitokea Januari mwaka huu jijini Tanga.
Alisema kuwa baada ya kumkamata mtuhumiwa huyo walimuhoji na kukiri kuwa alihusika katika kupora silaha pamoja na kushiriki kwenye tukio hilo pia ni miongoni mwa majambazi waliokuwa eneo la mapango ya mleni.
Aidha alikiri pia kuwepo ndani ya pango hilo wakati mapambano baina yao na Jeshi la Polisi na alikuwa ni mtu wa mwisho kutoka mapangoni humo akiwa na bunduki moja waliokuwa wameificha ndani humo.
Kaimu kamanda huyo alisema kuwa Machi 19 mwaka huu baada ya mtuhumiwa huyo kukamatwa saa mbili asubuhi aliwaongoza askari wa kikosi kazi Taifa wakiwa na Mkuuwa Upelelezi wa makosa ya Jinai Mkoa wa Tanga (RCO) kwenda kuwaonyesha silaha hiyo.
Alisema kuwa baada ya kufika mapangoni hapo walionyeshwa bunduki moja aina ya SMG yenye namba 14303545 ikiwa na risasi 29 ikiwa ni miongoni mwa bunduki walizoporwa askari Januari 26 mwaka huu.
Aidha alisema kuwa aliwaonyesha panga moja ,Begi moja la kaawia likiwa na nguo mbalimbali na mabomu matatu ya kutengeneza kienyeji ambazo walikuwa wakivutumia wakati wakijibizana na askari hao.
Aliongeza kuwa kupatikana kwa silaha hiyo kunafanya silaha zote mbili walizoporwa askari wa Jeshi hilo ambao walikuwa doria kupatikana

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »