Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo mara baada ya
kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mafia kuanza ziara ya siku mbili
wilayani humo tarehe 13.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akipokea ua kutoka kwa Mwalimu Mariam Halfan Haji mara baada ya kuwasili
kwenye uwanja wa ndege wa Mafia kama ishara ya upendo na kumkaribisha
rasmi kutembelea wilaya ya Mafia.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Hifadhi za Jamii (NSSF) Dkt. Ramadhan Dau alikuwa ni miongoni mwa
viongozi mbalimbali waliofika kwenye uwanja wa ndege wa Mafia kwa ajili
ya kumpokea Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alipowasili wilayani humo
tarehe 13.3.2013 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
Akina mama wa Mafia waliofika
kumpokea Mama Salma Kikwete wakati akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa
Mafia wanaonekana wakiwa wamebeba mabango ya kumkarisha wilayani humo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akimsalimia mtoto mwenye ulemavu wa ngozi/albino aliyekuwa amebebwa na
mama yake. Mama Salma alikutana na mtoto huyo wakati alipowasili kwenye
ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mafia.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Hifadhi za Jamii (NSSF) Dkt. Ramadhan Dau akitoa maelezo mafupi kuhusu
Shule ya Sekondari Bweni iliyoko katika Kata ya Kanga wilayani Mafia
ambayo imejengwa na “Mafia Island Development Foundation, MIDEF”. Dkt.
Dau ni mmoja wa viongozi wa Taasisi hiyo. Mama Salma alitembelea Shule
hiyo tarehe 13.3.2015. Waliokaa kutoka kushoto ni Mbunge wa Mafia
Mheshimiwa Abdulkarim Shah, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist
Ndikilo, Ndugu Mohamed Msosa, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo na mwisho ni
Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mafia.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bweni iliyoko katika Kata ya Kanga wilayani Mafia.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akiongea na wananchi wa Kijiji cha Bweni katika Kata ya Kanga waliofika
shuleni hapo kwa ajili ya kusalimiana naye.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akifurahia zawadi alizopewa na akina mama wajasiriamali wa Kata ya Kanga
huko Mafia mara baada ya kumaliza kuzungumza na wanafunzi na wananchi
wa eneo hilo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akizungumza na walimu wa Shule ya Sekondari Bweni iliyoko huko Mafia
mara baada kuongea na wanafunzi.
PICHA ZOTE NA JOHN LUKUWI