KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOANI ARUSHA

March 20, 2015

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kugonga kokoto pamoja na akina mama wajasiriamali katika kata ya Elerai mjini Arusha  wakati alipowatembelea  na kukagua shughuli zao,  ambapo aliwaambia “Asiwasumbue mtu wala kuwaambieni muondoke kwani ninawafahamu kwa muda mrefu toka nikiwa Mbunge wa jimbo hili  la Arusha mjini miaka ya nyuma”, aliwaagiza viongozi wa CCM wa kata hiyo kutojiingiza hata kidogo na kuleta mgogoro na wananchi hao ambao wanajitafutia rizki katika kazi yao hiyo.
Ameongeza kuwa CCM ni chama kinachotakiwa kuwasemea na kuwatetea wanyonge na siyo kuwakandamiza na kuwaonea  “Lazima viongozi na watendaji wa serikali na chama wawajibike kwa wananchi ambao ndiyo walioingia mkataba na CCM ambayo iliunda serikali inayotekeleza ilani yake” amesema .
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana yuko katika ziara ya kikazi ya mkoa wa Arusha akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, inayotekelezwa na serikali ya CCM huku akihimiza uhai wa Chama hicho akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-ARUSHA)2 
Kada wa CCM Viola naye akimwaga maneno ya sumu wakati wa mkutano wa katibu Mkuu wa Ndugu Abdulrahman Kinana na wafanya biashara wa soko la Kilombero jijini Arusha. 13 
Nape Nnauye akizungumza na umati wa wafanyabiashara na baadhi ya wananchi mbele ya jengo la Soko la Kilombero jijini Arusha. 14 
Baadhi ya wafanyabiashara na wananchi wakiwa katika mkutano huo. 15 
Kiongozi wa wafanyabiashara wa soko la Kilombero jijini Arusha akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana huku Nape Nnauye akiwa amemshikia kipaza sauti. 10 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »