Serikali inahitaji wamafundi sanifu 10,000 wa maabara (Laboratory Technicians) mpya zionazojengwa nchini.

March 20, 2015

001
Waziri wa TAMISEMI Mhe.Hawa Ghasia akijibu swali kwa niaba ya Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais na Menejimenti ya Utumishi wa Umma lililoulizwa na Mhe. Yahya Issa (Mb )wa Chwaka tarehe 20.03.2015.Mjini Dodoma.
…………………………………………………………………………………………
Na Anitha Jonas – MAELEZO,Dodoma.
Serikali imesema inauhitaji wamafundi sanifu 10,000 wa maabara(Laboratory Technicians) mpya zionazojengwa nchini.
Hayo yameyasema na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bungeni Mjini Dodoma, Mhe.Hawa Ghasia alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chwaka, Yahya Kassim Issa (CUF).
Katika swali lake Issa alitaka kujua kwa nini Serikali huwapa mikatabawatumishi waliostaafu wakati wapo vijana wengi ambao hawana kazi.
Waziri Ghasia alisema Serikali hutoa mikataba kwa baadhi ya kada ambazo bado hazijitoshelezi kutokana na kuwa na wataalamu wachache.

“Kwa mfano kwa sasa Serikali ina mahitaji makubwa wa mafundi sanifu wa maabara kwa ajili ya kusimamia maabara zetu zinazojengwa walipo kwasasa hawafiki 1,000 wakati mahitaji ni 10,0000,” alisema Ghasia.
Awali akijibu swali la Msingi la Mbunge huyo, Ghasia alisema sio seraya Serikali kuwaajiri wastaafu isipokuwa pale tu inapoonekana ni kwamanufaa ya umma kutokana na mahitaji makubwa katika sekta husika.
Alisema vijana na wasomi waliohitimu vyuo mbalimbali hapa nchini hupatiwa ajira kulingana na mahitaji ya bajeti iliyopo.
Waziri Ghasia alisema Kwa mujibu wa Kifungu cha 17 (1) cha Sheria ya Pensheni kwa Watumishi wa Umma sura namba 371, mtumishi wa umma anayo hiari ya kustaafu kwa hiyari akifikisha umri wa miaka 55.
003
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya wakiwa wamesimama ndani ya Bunge mara baada ya kutambulishwa kwa uwepo wao,Mjini Dodoma tarehe 20.03.2015.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »