Mkuu wa Mauzo na Masoko wa kampuni
ya Push Mobile Media Limited, Ezekiel Mukundi (Kulia) akielezea umuhimu
wa huduma ya “online bulk Messaging’ kwa sekta mbalimbali. Kushoto ni
Daniel Buchafwe ambaye ni Mkuu wa Idara ya Ufundi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Push Mobile
Media, Freddie Manento akifafanua jambo kuhusiana na huduma ya ‘Online
Bulk Messaging’ inavyofanya kazi. Huduma hiyo itamwezesha mtumiaji
kutuma ujumbe mmoja kwa watu wengi na katika muda muafaka.
……………………………………….
Na Mwandishi wetu
Kampuni inayoongoza kwa huduma
ya teknolojia ya mawasiliano, Push Mobile Media imezindua huduma ya
ujumbe kwa njia ya mtandao wa internet ijulikanyo kwa jina la “Bulk
Messaging” kwa lengo la kumwenzesha mtumiaji kufikisha ujumbe mmoja kwa
watu wengi na katika muda muafaka.
Akizungumza wakati wa uzinduzi
wa huduma hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Push Mobile Media, Freddie
Manento alisema kuwa huduma hiyo itamwezesha mtumiaji kufikisha ujumbe
muhimu kwa gharama nafuu ikiwa katika sekta mbalimbali na kwa mtu
binafsi.
Manento alisema kuwa lengo kubwa
ya kuanzisha huduma hiyo ni kuwawezesha wafanyabiashara na sekta
nyingine kufanya mawasiliano ya haraka zaidi na kujitangaza.
“Kama ni mfanyabiashara, utaweza
kujitangaza pia kwani wateja watapata taarifa muhimu utakazo wapa kwa
muda muafaka na wao kuutumia katika maendeleo ya biashara zao,” alisema
Manento.
“Ili kupata huduma hiyo, unatakiwa kujiunga kupitia mtandao wetu, www.pushgw.com na kufungua akaunti yako,” alisema Manento.
Alisema kuwa makampuni au
taasisi yanaweza kutumia huduma hii kuwapa taarifa wafanyakazi, wateja
wao kuhusiana na biashara na taarifa nyingine.
“Kwa watu binafsi, unaweza
kutumia huduma hii kutoa taarifa za shughuli mbalimbali ikiwa pamoja na
harusi na hata kwa waandishi wa habari wanaweza kutumia taarifa hii kwa
lengo la kuwasiliana na wahariri wao kwa kile wanachokifanya katika
sekta hiyo,” alisema.
Mkuu wa Idara ya Mauzo na Masoko
wa Push Mobile Media Limited Ezekiel Mukundi alisema kuwa huduma hiyo
ni rahisi kwani mtumiaji anaweza kutuma ujumbe kwa kiasi cha sh 16 kwa
kutegemea na ukubwa wa ‘bando’ analotaka.
Alisema kuwa kwa upande wa sekta
ya afya, huduma hii inawezwa kutumiwa na madaktari kuwakumbusha
wagonjwa kuhusiana na siku ya kupata matibabu.
“Unachotakiwa kufanya ni
kujiunga na huduma hii kwa njia ya mtandao na kuweka namba za simu ya
mkononi kwa watu wanaotakiwa kupata taarifa na kutuma, watapata kwa
haraka zaidi na kwa muda unaofaa,” alisema Mukundi.