Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira, Mheshimiwa Binilith Mahenge akisiliza jambo kutoka kwa
Mwenyeji wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bwana Abas Kandoro kabla ya kuanza
Ziara yake ya siku mbili Mkoani humo jana. (Picha na OMR)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira, Mh. Binilith Mahenge (katikati), wakijadili jambo na
Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mh. Deodatus Kinawito (kushoto) pamoja na
Diwani wa Kata ya Mkugani ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Wilaya ya Chunya, Mh. Bosco Mwanginde (kulia) wakati wa Ziara ya
Waziri Mahenge Wilayani humo jana.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira, Mh. Binilith Mahenge, akionesha Bwawa linalotumika
kuhifadhi Maji-taka yenye Sumu kutoka kwenye Mgodi wa Sunshine uliopo
Wilayani Chunya Mkoani Mbeya jana, huku akiwataka Wawekezaji wa Mgodi
huo kuboresha Bwawa hilo ili kukidhi Kanuni za Mazingira za Tanzania .
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira, Injinia Binilith Mahenge akisaini Kitabu cha Mahudhurio
ya Wageni mbele ya Mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bwana Abas
Kandoro, kabla ya kuanza ziara yake Mkoani humo jana .
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais, Injinia Binilith Mahenge (kushoto), akizungumza na Mkurugenzi
Msaidizi wa Machimbo ya Dhahabu katika Mgodi wa Sunshine uliopo Wilayani
Chunya, Bwana Andy Wu (kulia), katika ziara ya Mazingira Mgodini humo
jana na wakati katika picha ni Diwani wa Kata ya Mkugani ambaye pia ni
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya, Mh. Bosco Mwanginde.