Taarifa kutoka Kenya kuhusu kuzuiwa Magari kutoka Tanzania kuingia mbugani, viwanja vya ndege

February 06, 2015

safari2-2
Mvutano katika ishu ya utalii  imeendelea kuingia kwenye headlines kubwa leo, vyombo vya habari Kenya vimeripoti ishu ya Serikali ya Kenya kupiga marufuku magari ya kitalii kutoka Tanzania kuingiza watalii katika mbuga za wanyama na viwanja vya ndege vya nchi hiyo.
Waziri wa Masuala ya Jumuia ya Afrika na Utalii nchini humo, Phyllis Kandie ametangaza kutekelezwa kwa hatua hiyo mara moja  hadi pale mzozo uliyopo kati ya nchi hizi mbili juu ya masuala ya utalii utakapomalizika.
.
Phyllis Kandie
Waziri huyo amesema kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya mataifa haya mawili kushindwa kufanya kikao maalum kama ilivyotegemewa baada ya muda wa wiki tatu uliokuwa umepangwa kuisha.
024-lioness 
Kwa sasa magari ya watalii nchini Tanzania yataruhusiwa kuingia nchin i humo lakini yanatakiwa yawe na leseni, ingawa Kenya imeruhusu magari ya watalii kuingia maeneo yote nchini humo, kwa upande wa Tanzania imeruhusu magari ya kitalii kutoka Kenya kuingia katika mikoa ya Tanga, Moshi, Arusha na Musoma.
Sikiliza taarifa hiyo iliyoripotiwa na kituo cha K 24 kutoka Kenya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »