MAKAMU WA RAIS AONGOZA MAELFU KATIKA MAZISHI YA WATU SITA WA FAMILIA MOJA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MOTO

February 10, 2015

 Mama mzazi wa Kapteni David Mpila akiweka udongo katika kaburi la mtoto wake marehemu David Mpila leo wakati wa mazishi ya watu sita waliokufa kwa ajali ya moto baada ya nyumba yao kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia Februari 7.
 Waombeleji wakielekea makaburini.
 Baadhi ya watu wakielekea makaburini.
 Wanafamilia wakiwa na huzuni baada ya miili kuwasili nyumbani
 Miili ikiwasili nyumbani.
 Miili ikiombewa nyumbani kabla ya kuelekea makaburini kwa mazishi.
 Mpumzike kwa amani.
  Makamu wa rais, Dk. Mohamed Ghalib Bilali akitoa heshima za mwisho mbele ya majeneza yaliyokuwa na miili ya watu sita wa familia moja waliofariki kwa ajali ya moto.
Mofisa wa Jeshi la wananchi wa tanzania (JWTZ) wakitoa heshima za mwisho.

Majeneza yenye miili ya watu sita wa familia moja waliofariki kwa ajali ya moto baada ya nyumba yao kuteketea kwa moto eneo la Kipunguni ‘A’ jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Februari 7, ambao walizikwa katika makaburi ya Airwing Ukonga, Dar es Salaam leo.

 Tutawakumbuka daima......
 Askari wa JWTZ wakiwa wamebeba moja ya jeneza la marehemu waliofariki katika ajali ya moto wakati wa mazishi yao.
 Fatuma Issa ambaye ni mama wa watoto wawili waliofariki katika ajali hiyo akiweka udongo katika makaburi la watoto wake.
 Mtoto pekee aliyenusurika katika ajali hiyo, Emmanuel mpila akiweka udongo katika kaburi la baba yake, Kapteni mstaafu wa JWTZ, David Mpila.
 Mama mzazi wa Kapteni David Mpila akiweka shada la maua.
 Fatuma Issa akiweka shada la maua katika makaburi ya watoto wake Celina na Pauline.
 Mama wa watoto wawili waliofariki katika ajali ya moto, Fatuma Issa akiweka shada la maua katika kaburi la mtoto wake, Celina.
 Emmanuel Mpila akiweka shada la maua katika kaburi la mototo wake, Pauline, Emmanuel alipoteza wa toto wawili katika ajali hiyo.

 Baba wa watoto wawili waliokufa katika ajali ya moto, Emmanuel Mpila akiweka shada la maua katika kaburi la mmoja wa watoto wake, Pauline
.

 Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal akiweka shada la maua.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akiweka shada la maua.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Mark Mwandosya akiweka shada la maua.
 Jaji Mkuu mstaafu, Agustino Ramadhani akiweka shada la maua.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwenye majeneza yenye miili ya Familia ya marehemu Kapten David Mpila waliofariki kwa kuteketea na moto nyumbani kwao Kipunguni, wakati wa mazishi yao yaliyofanyika leo Februari 10,2015 katika makaburi ya Airwing Ukonga              Dar es salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimfariji mama mzazi wa marehemu bibi Celina Mpila mke wa marehem Kapten David Mpila waliofariki kwa kuteketea na moto, wakati wa mazishi yao yaliyofanyika leo Februari 10,2015 katika makaburi ya Airwing Ukonga Dar es salaam.  

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »