Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Charles Kitwanga, (Kushoto)
akimkabidhi tuzo mshindi wa Tuzo za Bodi yenye Uongozi Bora za 2014
(BBLA) katika sekta ya kibenki, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya
Benki ya CRDB Bw. Martin Mmari (kulia). Benki ya CRDB iliibuka mshindi
katika sekta ya kibenki wakati kampuni ya Heritage Insurance iliibuka
kinara katika sekta ya bima katika tuzo hizo zilizofanyika jijini Dar
es Salaam.
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Charles Kitwanga, (Kushoto)
akimkabidhi tuzo mshindi wa Tuzo za Bodi yenye Uongozi Bora za 2014
(BBLA) katika sekta ya bima, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya
kampuni ya Heritage Insurance, Bw. Yogesh Manek (kulia). Heritage
Insurance iliibuka mshindi katika sekta ya bima wakati Benki ya CRDB
iliibuka kinara katika sekta ya kibenki katika tuzo hizo.
Mwenyekiti wa jopo la majaji
waliosimamia Tuzo za Bodi yenye Uongozi Bora za 2014 (BBLA), Bw. Leonard
Mususa akizungumza katika hafla ya kutangaza washindi wa tuzo hizo
ambapo kampuni ya bima ya. Heritage iliibuka mshindi katika sekta ya
bima wakati Benki ya CRDB iliibuka kinara katika sekta ya kibenki katika
tuzo hizo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini,
Mhe. Charles Kitwanga akizungumza katika hafla ya kutangaza washindi
wa Tuzo za Bodi yenye Uongozi Bora za 2014 (BBLA), ambapo kampuni ya
bima ya. Heritage iliibuka mshindi katika sekta ya bima wakati Benki ya
CRDB iliibuka kinara katika sekta ya kibenki katika tuzo hizo.
Picha mpiga picha wetu.