JONAS MKUDE AZITOSA YANGA SC NA AZAM FC NA KUJIFUNGA SIMBA SC

November 06, 2014
Na Baraka Mbolembole,
Kiungo wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Jonas Mkude amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea klabu yake ya Simba. Mkude, 21 ni moja ya matinda ya kikosi cha pili cha mabingwa hao mara 19 wa kihistoria wa Tanzania Bara, amepatiwa gari aina ya Toyota GX 115, huku pia kiwango chake cha mshahara kikipanda.
Mchezaji huyo wa nafasi ya kiungo ambaye atafikisha miaka 22 Disemba 3, ni mchezaji muhimu katika timu hiyo na alikuwa akihusishwa na mpango wa kusajiliwa na klabu ya Yanga SC na Azam FC lakini kitendo cha kusaini klabu iliyomlea ni kama kumaliza mbio za timu hizo ambazo zilionesha nia ya kumuhitaji kiungo huyo wa ulinzi.
8
Habari za ndani kutoka klabu ya Simba zinadai kuwa kiungo raia wa Burundi, Pierre Kwizera anaweza kutemwa klabuni hapo baada ya kuonyesha kiwango cha chini huku akishindwa kuendana na uchezaji wa timu hiyo. Kwizera ni mzuri katika kupanga mashambulizi pekee, wakati Mkude anaweza kukaba na kuichezesha timu. Wote wawili hucheza kama viungo wa chini na ili kuendelea kuijenga timu hiyo, Simba imeona ni bora kumuongezea mshahara, na kumpatia kile alichokuwa akihitaji Mkude kwa kuwa wataendelea kupata huduma nzuri..

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »