RPC KASHAI AELEZA CHANZO CHA MADUKA MANNE KUTEKETEA WILAYANI KILINDI.

October 13, 2014
NA MWANDISHI WETU,KILINDI.
IMEELEZWA kuwa chanzo cha tukio la kuungua moto nyumba mmoja yenye fremu nne za maduka wilayani Kilindi mkoani Tanga ilisababishwa na moto ulikuwa ukitumiwa na mama lishe jirani eneo hilo kusambaa kwenye maeneo yaliyopo sheli hiyo na kuunguza eneo hilo.

Moto huo uliachwa bila kuzimwa baada ya mamalishe hao kumaliza biashara zao za kuuza chakula jambo ambalo lilipelekea kuleta hasara kubwa kwenye maduka hayo ambapo thamani yake bado haijajulikana mpaka sasa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Fresser Kashai alithibitisha kutokea tukio hilo ambapo alisema lilitokea Octoba 7 mwaka huu katika kijiji na kata ya Negero Tarafa ya Kimbe wilayani humo .

Akielezea jinsi tukio hilo lilivyotokea Kamanda Kashai alisema kuwa gari lenye namba za usajili T.219 AUC Center yenye tanki la mafuta linalomilikiwa na Adolf Lykundi mkazi wa Handeni lilishika moto na kulipuka wakati likimimina mafuta ya petrol kwenye mapipa dukani kwa Majaaliwa Songomelo.

Hata hivyo,Kamanda Kashai alisema kuwa katika tukio hilo hakuna madhara yaliyotokea kwa binadam.

Wakati huo huo,mkazi mmoja wa Kijiji cha Mafisa Kata ya Mvungwe Tarafa ya Mgera wilayani Kilindi ameuwawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya Tumboni, Shingano na Kichwani hali iliyopelekea kufariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Fresser Kashai alithibitisha kutokea tukio hilo ambalo lilitokea Octoba 7 mwaka huu saa 11:30 Marehemu akiwa shambani kwenye kitongoji baina ya Kijiji cha Mafisa wilayani humo.

Kamanda Kashai alimtaja alifariki dunia kwenye tukio hilo kuwa ni Lokoye Machaku (29) kabila Mnguu mkazi wa Maafisa wilayani humo ambayo alichomwa kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali kwenye mwili wake.

Aidha alisema kuwa wakati huo mtu mwengine aliyekuwa ameongozana na marehemu Mohamed Mhina (35) mkazi wa eneo hilo alijeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali katika mkono wake wa kulia.

Kamanda Kashai alisema kuwa tukio hilo lilifanywa na watu wawili wa jamii ya wafugaji na walikuwa wamevaa nguo za kimasai na inasadikiwa kuwa ni wakazi wa kijiji cha Lembapuri wilayani Kiteto mkoani Manyara.

Alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kugombania malisho ambapo watuhumiwa walilisha mifugo yao kwenye shamba la mabua yaliyokuwa shambani baada ya mavuno katika eneo hilo la mafisa.

Hata hiyo alisema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Kilindi kwa ajili ya uchunguzi wakati jeshi hilo linaendelea na msako mkali kuwatafuta wahalifu waliohusika kwenye tukio hilo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »