Timu ya kuvuta kamba ya
wanawake ya Ikulu wakiwavuta timu ya Wizara ya Kilimo, Ushirika na Chakula
(hawapo pichani) wakati wa mashindano ya kuingia hatua ya nusu fainali
mashindano ya SHIMIWI leo mjini Morogoro
ambapo Ikulu imefuzu kucheza hatua hiyo.
Timu ya kuvuta kamba ya wanaume ya Ikulu
wakiwavuta timu ya Wakala wa Hifadhi ya Chakula ya Taifa (NFRA- hawapo pichani)
wakati wa mashindano ya kuingia hatua ya nusu fainali mashindano ya SHIMIWI leo
mjini Morogoro ambapo Ikulu imefuzu kucheza hatua hiyo.
Mshindi wa kwanza wa mchezo wa drafti wanaume
Salumu Simba (kushoto) kutoka RAS Dodoma akichuana na mshindi wa tatu wa mchezo
huo Ramadhani Mtenga (kulia)kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo wakati wa mashindano ya SHIMIWI leo mjini Morogoro.
Mshindi wa kwanza wa
mchezo wa drafti wanaume Salumu Simba (kulia) kutoka RAS Dodoma akichuana na
mshindi wa tatu wa mchezo huo Dkt. Idris Lukindo (kushoto) wakati wa mashindano
ya SHIMIWI leo mjini Morogoro.
Baadhi ya watumishi
wanaoshabikia mchezo wa drafti wakishuhudia pambano la kuwatafuta washindi wa mcheo huo leo katika kiwanja cha Jamhuri mjini
Morogoro.
Mchezaji wa timu ya
mpira wa pete Ikulu Mwadawa Twalibu (GA) akimiliki mpira wakati wa mchezo wa
robo fainali kati ya timu ya Ikulu na Bunge wa kumsaka mshindi atakayecheza
nusu fainali, timu ya Ikulu imefuzu kwa kuwashinda timu ya Bunge kwa magoli 67
kwa 24.
Wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (waliovalia sare ya bluu) wakisalimiana na
wachezaji wa mchezo huo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (waliovalia sare ya rangi
ya machungwa) kabla ya mchezo wa robo fainali ambapo timu ya Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo wameibuka washindi na kuingia nusu fainali katika
mshindano ya SHIMIWI kwa kuifunga timu ya Ofisi ya Waziri Mkuu 1- 0.
Timu ya mpira wa miguu
ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (kushoto) na timu ya Ofisi ya
Waziri Mkuu (kulia) wakiomba dua kabla ya mchezo wa hatua ya robo fainali leo
mjini Morogoro.
Baadhi ya watumishi wa
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakishangilia ushindi wa timu
yao wa kuifunga timu ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa goli 1- 0 leo mjini Morogoro. Picha zote na Eleuteri
Mangi- MAELEZO
**************************************
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Michuano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI)
imefikia hatua ya nusu fainali kwa michezo ya kuvuta kamba, mpira wa miguu na
mpira wa pete kwenye mashindano yanayoendelea mjini Morogoro.
Katika mchezo wa kuvuta kamba timu za wanaume zilizoingia hatua hiyo ni
Ikulu, Uchukuzi, Hazina na Mahakama wakati kwa upande wa wanawake timu
zilizoingia hatua hiyo ni Ikulu,
Uchukuzi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na
RAS Iringa.
Kwa upande wa mpira wa pete timu zilizofuzu ni Ikulu, Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii, Wizara ya Uchukuzi na timu ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma.
Wakati huo huo, timu zilizokata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali kwa
mpira wa miguu ni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Wizara ya
Uchukuzi, Idara ya Mahakama na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Aidha, mchezo wa drafti umefikia ukingoni ambapo kwa wanaume bingwa wa
mchezo huo imedchukuliwa na Salumu Simba kutoka timu ya RAS Dodoma, nafasi ya
pili imekwenda kwa Dkt. Idris Lukindo kutoka Wakala wa Jiolojia
Tanzania (GST) na nafasi ya tatu imekwenda
kwa Ramadhani Mtenga kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Kwa upande wa wanawake,
Leocadia Mwang’ombe kutoka RAS Morogoro ameibuka bingwa kwa mchezo wa drafti
huku nafasi ya pili imekwenda kwa Sophia Mpema kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi na nafasi ya tatu imeenda kwa Madaraka Kabaka kutoka RAS Mwanza.