MASHAMBULIZI MENGINE YA JAMIE CARRAGHER KWA ARSENAL HAYA HAPA...

September 20, 2014


Arsenal were defeated 2-0 in Dortmund on Tuesday, but it could have been much more for the Germans
Arsenal walifungwa 2-0 na Dortmund siku ya jumanne, lakini bado wana imani kubwa ya kufanya vizuri

BADO ni mapema mwa msimu, lakini tayari kuna maswali ya kujiuliza kuhusu Arsenal. Swali kubwa ninalohisi ni hili hapa: Kipi kinabadilika?
Kwa kuwatazama dhidi ya Borrussia Dortmund jumanne usiku, isingewezekana kuhitimisha kwamba, Arsenal hawajifunzi.
Kwa muongo mmoja sasa, Arsenal wamekuwa wakishindwa kupambana na timu inayocheza mpira wa kasi na mpango wa kutumia nguvu. Kila mtu anajua jinsi ya kucheza nao.
Danny Welbeck has been brought in from Manchester United, but is yet to score after a host of chances
Danny Welbeck amesajiliwa kutoka Manchester United, lakini bado amekuwa na ugonjwa wa kukosa nafasi za magoli.

Dortmund wangeweza kufunga mabao kirahisi kama walivyofanya Liverpool (5-1 mwezi februari) na Cheslea (6-0 mwezi machi), lakini kitendo cha kutofungwa mechi 29 za ugenini katika michuano ya UEFA, kiukweli ni rekodi nzuri mno kwa Arsenal.
Ninapoitazama Arsenal kwasasa, ninachanganyikiwa. Wanacheza vilevile kila wanapokwenda- mabeki wao wa pembeni wanapanda juu na kutanuka- na hufungwa kwa mashambulizi ya kushitukiza.
Wao ni wageni! wangekuwa wanafanya hivyo wakiwa nyumbani. Kwanini hawajifunzi?
Nilipokuwa naichezea Liverpool, lengo la kwanza siku zote lilikuwa kutofungwa: Tulijilinda sana na kama nafasi inatokea basi tuliitumia haraka. Kama mashabiki wa nyumbani hawakupenda, maana yake ilikuwa nini?
Bado Arsenal wanaamini wanaweza kuifunga timu yoyote na popote pale wakicheza mpira wao. Ni vibaya sana. Timu pekee iliyoweza kushinda ugenini kwa miaka ya karibuni kwa staili hii ni Barcelona ya Pep Guardiola. Moja ya timu kubwa zaidi miaka ya karibuni, lakini alionekana kuja na mbinu nyingine za kutafuta matokeo.
Angalia mabingwa wa mwaka jana wa UEFA, Real Madrid, walifuzu fainali kwa kushambulia kwa kushitukiza dhidi ya Bayern Munich-na hii ilikuwa katika mchezo wa kwanza Bernabeu. Ilikuwa mbinu nzuri kwao.
Kufanya mambo tofauti ni jambo la msingi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »