WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA KATIKA MAADHIMISHO YA NANENANE NYANDA ZA JUU KUSINI JIJINI MBEYA LEO

August 02, 2014


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akisalimiana na
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Adam Misana
alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya hiyo leo tarehe 02/08/2014 katika
maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya ambapo
alipokelewa na viongozi waandamizi wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa wakiongozwa na
Mkuu wa Mkoa huo Eng. Stella Manyanya (Pichani Kulia).
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda (aliyeshika boga
kushoto) akisikiliza maelezo ya kilimo bora cha maboga alipotembelea banda la
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya
wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya. Kulia kwake ni Waziri
Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Merry Nagu na pichani kulia
ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akipokea maelezo
kutoka kwa mjasiriamali kuhusu kilimo cha Uyoga alipotembelea banda la
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima
Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya.  Wa pili kushoto ni mwanasiasa nguli nchini na
Mbunge wa zamani wa jimbo la Kwela Dkt. Chrissant Mzindakaya.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda wa pili kushoto
akiangalia mbegu ya uyoga alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya
Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda
za juu kusini Jijini Mbeya. Wa kwanza kushoto ni mwanasiasa nguli nchini na
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kwela Dkt. Chrissant Mzindakaya na wa pili kulia
ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya.
Kilimo cha uyoga ni rahisi kwani sio lazima uwe na shamba, kama unavyoonekana pichani.
Picha ya pamoja kati ya Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda, viongozi wa serikali mkoani
Rukwa na wajasiriamali wadogowadogo mara baada ya kutembelea banda la
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya
wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »