Timu
ya Tanzania ya umri chini ya miaka 15 imewasili salama jijini Gaborone,
Botswana kwa ajili ya michezo ya Afrika ambapo itacheza mechi yake ya kwanza
Mei 22 mwaka huu dhidi ya Mali.
Kikosi
hicho cha wachezaji 16 chini ya Kocha Abel Mtweve kimetua jijini Gaborone jana
(Mei 19 mwaka huu) jioni kwa ndege ya South African Airways. Michezo hiyo itamalizika
Mei 30 mwaka huu.
Wachezaji
waliopo kwenye kikosi cha Tanzania ni Adam Shayo, Amani Ally, Amos Manguli,
Amri Nyuki, Amede Amani, Baraka Rashid, David Uromi, Goodlove Mdumule, Hance
Msonga, Kelvin Kamalamo, Makalius Amrin, Nasson Chanuka, Paulo Ngowi, Petro
Shaban, Rajab Mohamed na Thomas Chindeka.
Nchi
nyingine zinazoshiriki michezo hiyo kwa upande wa mpira wa miguu ni Afrika
Kusini, Botswana, Nigeria, Mali na Swaziland.
Gabon
na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) ambazo nazo zilikuwa zishiriki kwenye
michezo hiyo katika dakika za mwisho.

EmoticonEmoticon