*WATUMISHI WA SERIKALI NA MASHIRIKA YA UMMA WAFANYA TAMASHA LA MICHEZO KUADHIMISHA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

April 14, 2014

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Michezo na Burudani kuelekea maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Bw. Leonard Thadeo wakwanza kulia akiongoza tamasha la mazoezi ya viungo kwa Watumishi wa Serikali na Mashirika ya Umma mapema wikiendi hii katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,Tamasha hilo ni muendelezo wa program mbalimbali za kuadhimisha Muungano kwa njia ya Mchezo na Burudani.
 Baadhi ya watumishi wa Serikali na Mashirika ya Umma wakiwa katika tamasha la michezo katika kuadhimisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mapema mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa wizara ya Habara, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Barnabas Ndunguru(kushoto) na Afisa Tawala wa Wizara hiyo Bw. Mussa Varisanga wakifanya mazoezi wakatio wqa Tamasha la mchezo kwa ajili ya kuadhimisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika mapema mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mtumishi kutoka Wizara ya Ulinzi Bw. Abdul Nyumba akiwaongoza watumishi wenzake katika mazoezi ya viungo mapema mwishoni mwa wiki wakati wa Tamasha la Michezo kwa ajili ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Michezo na Burudani kuelekea maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Bw. Leonard Thadeo akizungumza na watumishi kutoka wizara mbalimbali na mashirika ya Umma walioshiki tamasha la michezo kwa ajili ya kuadhimisha Muungano mapema wikiendi hii. Picha na Frank Shija.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »