*MAANDALIZI KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 37 YA CCM MKOANI MBEYA KESHO
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kupalilia katika shamba la
Mage Kolimwa (wapili kulia), katika Kijiji cha Mlimanyoka, Kata ya
Nsalanga, wilala ya Mbeya mjini. Kinana alifika kumsaidia mkulima huyo
ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, inayofanyika Kitaifa
Jumapili hii mjini Mbeya.
Katibu
wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisaidiana na vijana kuandaa
jukwaa litakalotumika wakati wa mapokezi ya matembezi ya maadhimisho ya
miaka 37 ya CCM, kwenye Uwanja wa Sokine mjini Mbeya. Matembezi hayo
yanaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete
Vijana wakiwa kwenye mazoezi ya maadhimisho ya miaka 37 ya CCM yatakayofanyika Jumapili hii mjini Mbeya.