Kocha wa Yanga,Hans Van Der Pluijm kulia akitoka kwenye uwanja wa Mkwakwani leo asubuhi mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu hiyo kushoto ni Ofisa Habari wa timu hiyo,Baraka Kizuguto.
TIMU ya Dar es Saalam Yanga Africa imetua jijini Tanga juzi
na kulakiwa na wapenzi pamoja na wanachama wao wakiwa na matumaini makubwa
kuweza kuibuka na ushindi kwenye mechi yao dhidi ya Coastal Union ya Tanga kesho
Mchezo huo unaotarajiwa kupigwa kwenye dimba la CCM
Mkwakwani unatarajiwa kuwa mkali na upinzani wa hali ya juu kutokana na
timu zote kufanya maandalizi nje ya nchi kwa Yanga kwenda Uturuki na Coastal
Union wao wakitokea Omani.
Yanga wao waliwasili mkoani Tanga juzi wakitokea jijini Dar
es Salaam wakiwa wachezaji wao 20 ambao watatumika kwenye mechi hiyo na
kufanya mazoezi kwenye viwanja vya Gymkana na CCM Mkwakwani wakiwa na idadi
kubwa ya mashabiki waliojitokeza kuwaona wachezaji mahiri wa timu hiyo.
Mazoezi ya timu hiyo yalikuwa yakiongozwa na Kocha Mkuu wa
timu hiyo, Mholanzi Hans Van Der Pluijm akisaidiana na Charles Boniface Mkwasa
na Juma Pondamali “Mensa”ambayo yalikuwa wakianza saa moja asubuhi mpaka saa
tatu asubuhi.
Akizungumzia mechi yao na Coastal Union ya Tanga, Hans Van Der
Pluijm alisema alichofuata mkoani hapa ni kuhakikisha anachukua pointi tatu na
sio kitu kingine kwani wachezaji wake wana kiwango kizuri ambacho kinafanikisha
malengo yake hayo.
Kocha huyo alisema msimu huu matarajio yake makubwa ni
kutaka kuendelea kuchukua ubingwa wa Ligi kuu Tanzania bara akisema hilo
linawezekana kutokana na uongozi imara na mshikamano uliopo kwenye klabu hiyo.
Hata hivyo Kocha huyo aliwataka wachezaji wake kutumia akili
wanapokuwa mchezoni pamoja na kucheza pasi ndefu kwani hiyo ndio silaha ya
ushindi kwenye mechi zao kwenye mzunguko huo wa pili wa ligi kuu hapa nchini.
“Mnapaswa
kubadilika na kucheza pasi ndefu ndefu pamoja na kutumia akili pindi muwapo
mchezoni kwani aina hivyo inaweza kutupa mafanakio makubwa sana siku za mbele
kwenye michuano hii “Alisema Mholanzi Van Der Pluijm.
Wakati Yanga wakiwa Uwanja wa CCM Mkwakwani wapinzani wao
Wagosi wa Kaya “Coastal Union” wao wanafanya mazoezi kwenye dimba la soka
Gymkan wakiwa na matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo
Msemaji wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Hafidhi Kido aliliambia
gazeti hili kuwa mechi hiyo haitakuwa rahisi sana kama watu wengi wanavofikiria
kwa sababu wao wamedhamiria kuhakikisha wanapata pointi tatu na hilo
litawezekana kutokana na kuimarika kikosi hicho.
“Mechi hii ni ngumu
hivyo tutahakikisha tunashinda ili tuwafunge midomo Yanga na hili ndilo ambalo
litadhihirisha kuwa hatukwenda Omani kutalii bali kuweka kambi “Alisema Kido.
Aidha kwa upande mwengine, Mashabiki wa Coastal Union
wameitabiria timu yao ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Yanga kwenye mechi hiyo wakisema
wanaamini kikosi kimekamilika kwa asilimia.
Hali ya Jiji la Tanga imeonekana kubadilika kwa pilika
pilika kuelekea mchezo huo huku baadhi ya mashabiki na wapenzi wakiwa kwenye
maeneo mbalimbali wakinunua tisheti za timu hizo mbili wakati wengine wakinunua
zile za Simba.
EmoticonEmoticon