Na Oscar Assenga, Tanga.
JUMLA ya wahamiaji haramu 590
walikamatwa mkoani Tanga katika kipindi cha
kuanzia Januari 2012 hadi octoba 2013 kutokana sababu mbalimbali ikiwemo
kuingia nchini bila kibali na kufanya kazi.
Takwimu hiyo ilitolewa na
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa wakati akitoa taarifa ya
mafanikio ya mkoa wa Tanga mwaka 2012 hadi Octoba 2013 kwa vyombo vya habari
mwishoni mwa wiki.
Gallawa alisema kipindi cha
kuanzia Januari hadi Desemba 2012 jumla ya watuhumiwa 289 wa mataifa ya
Ethiopia 116,Kenya 53,Uganda 29,Switzerland 1,India 6,Italia 1,German 4,Afrika
Kusini 3,Somalia 18,Portugues 1,Bangladesh 2,Denmark 1,Zambia 2,China 2,Congo1.
Aidha aliongeza kuwa
wahamiaji haramu waliokamatwa kutoka mataifa mengine ni Guinea 1,Turkey
1,Sri-Lanka 1,Pakistan 6,Peru 1,Egypt
1,Norway 2 na watanzania 32 ambao walikamatwa kwa makosa yaliyotajwa hapo juu
ukilinganisha na kipindi cha kuanzia Januari hadi Octoba 2013 ambapo jumla ya
watuhumiwa 301 kutoka nchi mbalimbali
waliokamatwa.
Gallawa alisema katika
kipindi hicho wahamiaji haramu kutoka nchini Ethiopia 213,Kenya 29,India
9,China 3,Bangladesh 7,Djibout 1,Pakistan 1,Burundi 1,Somalia 2,British
2,Osterech 1,Uganda 2,Israel 2,USA 2 na watanzania 25.
Aliongeza kuwa takwimu hizo
zinaonyesha idadi ya wahamiaji haramu hasa raia wa Ethiopia waliokamatwa imeongezeka
kati ya mwaka 2012 hadi kufikia Octoba 2013 .
Mkuu huyo wa mkoa alisema
idadi ya watanzania waliokamatwa kwa kosa la kusaidia au kuwahifadhi na
kuwasafirisha wahamiaji haramu imepungua ukilinganisha na kipindi cha mwaka
2012.
Alisema takwimu hizo ni
mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa idara ya uhamiaji Tanga kwa kutoa elimu
kwa wananchi juu ya athari zitokanazo na wahamiaji haramu na ushirikishwaji wa
wananchi dhidi ya mapambano ya kudhibiti wimbi la wahamiaji haramu nchini.
Hatua zilizochukuliwa dhidi
ya wahamiaj haramu hao ni kufikishwa mahakamani pamoja na kufukuzwa nchini kwa
kupewa notisi.