KAJALA MASANJA KUTOKA NA FILAM MPYA YA LAANA MWEZI FEBRUARI
MSANII
wa filam za Kibongo nchini, Kajala Masanja, yupo katika hatu za mwisho
za maandalizi ya kuanza kurekodi filamu yake mpya inayokwenda kwa jina
la 'Laana', inayotarajia kukamilika mwezi Februari mwaka huu.
Akizungumza
na mtandao huu wa www.sufianimafoto.com, Kajala alisema kuwa hivia sasa
wapo katika maandalizi ya kuanza kurekodi filamu hiyo,
itakayowashirikisha wakali kibao wa movie za Kibongo.
Aidha
Filamu hiyo inayoanza kurekodiwa wiki ijayo chini ya Kampuni ya Sophia
Records, inatarajia kukamilika na kuzinduliwa na kuingia sokoni mwishoni
mwa mwezi wa pili.
Kajala
aliwataja baadhi ya wasanii watakaoshiriki katika Filamu hiyo
iliyotungwa na Leah Richard, kuwa ni Gabo, Lutwaza, Mama Kawele, ambapo
Sterling wa Filam hiyo atakuwa ni Kajala, Gabo na Mama Kawele.
Kajana akipozi kwa 'Snap' baada ya mazungumzo na Sufianimafoto.