January 02, 2014

KAJALA MASANJA KUTOKA NA FILAM MPYA YA LAANA MWEZI FEBRUARI

MSANII wa filam za Kibongo nchini, Kajala Masanja, yupo katika hatu za mwisho za maandalizi ya kuanza kurekodi filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la 'Laana', inayotarajia kukamilika mwezi Februari mwaka huu.

Akizungumza na mtandao huu wa www.sufianimafoto.com, Kajala alisema kuwa hivia sasa wapo katika maandalizi ya kuanza kurekodi filamu hiyo, itakayowashirikisha wakali kibao wa movie za Kibongo.

Aidha Filamu hiyo inayoanza kurekodiwa wiki ijayo chini ya Kampuni ya Sophia Records, inatarajia kukamilika na kuzinduliwa na kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi wa pili.

Kajala aliwataja baadhi ya wasanii watakaoshiriki katika Filamu hiyo iliyotungwa na Leah Richard, kuwa ni Gabo, Lutwaza, Mama Kawele, ambapo Sterling wa Filam hiyo atakuwa ni Kajala, Gabo na Mama Kawele. 
Kajana akipozi kwa 'Snap' baada ya mazungumzo na Sufianimafoto.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »