SIMBA WAICHAPA YANGA BAO 3-1

December 21, 2013
 Wachezaji wa Simba na baadhi ya viongozi wao wakipozi na kombe lao kwa furaha baada ya kukabidhiwa kombe hilo kwa kuifunga Yanga katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Simba wameibuka washindi kwa.kuichapa Yanga mabao 3-1, mabao ya Simba yalifungwa na Hamis Tambwe mawili na Ramadhan Singano huku la kufutia machozi la Yanga likifungwa na Emmanuel Okwi.
 Meneja wa Yanga, Afidh Ally akipokea mfano wa hundi ya zaidi  sh. 98 milioni Kwa kuibuka washindi katika shindano la Nani Mtani Jembe kwa kupata kura nyingi katika unywaji wa bia ya Kilimanjaro.
Kiongozi wa Simba Hans Pope, akimpongeza Henry Joseph, baada ya mchezo huo. Kaa na ukurasa huu kwa matukio zaidi ya mchezo huu yatakayokujia hapo baadaye.
 Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, akiruka hewani kushangilia bao la kwanza la Simba lililofungwa na Hamis Tambwe katika dakika ya 14, ya kipindi cha kwanza.
 Mshambuliaji wa Simba Hamis Tambwe, akifunga bao la pili kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 44, baada ya beki wa Yanga, David Luhende kumkwatua Ramadhan Singano katika eneo la hatari.
Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu, akijaribu kumfinya beki wa Simba, Joseph Owino wakati wa mtanange huo. Mpira sasa ni kipindi cha pili.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »