MASHUJAA BENDI KUWASHA MOTO TANGA JANUARI 11

December 21, 2013


Na Oscar Assenga,Tanga.
BENDI ya Mziki wa Dansi nchini Mashujaa yenye makazi yake jijini Dar es Salaam inatarajiwa kufanya onyesho la aina yake Januari 11 mwakano mkoani hapa amblo litafanyika ukumbi wa Nyumbani Hotel.

Onyesho hilo limeandaliwa na Kampuni ya New Face kwa kushirikiana na Mashujaa Band lenye lengo la kuwapa burudani wakazi wa Tanga  na kuzitambulisha tuzo 5 walizopata wakati wa Kilimanjaro Music Award.

Akizungumzia maandalizi ya Onyesho hilo,Mkurugenzi wa Kampuni ya New Face Intertainment,Maximilian Luhanga alisema kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa na kinachosuburiwa na siku ya onyesho hilo kufanyika.

Luhanga alisema kuwa wasanii nguli wa band hiyo akiwemo Charles Baba watawakonga nyoyo mashabiki wao kwa kutoa burudani ya aina yake siku hiyo wakiwa sambamba na Furgson,

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »