Raisa Said,Korogwe
MJUMBE wa
Halmashauri kuu CCM Taifa {NEC}
Kupitia Jimbo la
Korogwe vijijini Dr. Edmund Mndolwa ameahidi kutoa
mil. 5 kwa vijana ambao wataandaa ekari tano
za shamba la kulimia alizeti lengo
likiwa kuwakwamua kiuchumi.
Akizungumza katika
mikutano mbalimbali wakati wa ziara
yake ya siku
za saba jimboni humo alisema
ameahidi kutoa pesa
hiyo kwa vijana
wakata 20 ambao
wataandaa maeneo
ya kulimia alizeti.
Dk
Mndolwa ambae pia ni
mwenyekiti wa Wazazi
Mkoa wa Tanga alisema
kuwa mpango huo
utaweza kuwasaidia vijana wengi
kujiajili na kuepuka
kufanya vitendo viovu
na kuacha kukaa vijiweni bila
ajira.
Mjumbe
huyo wa Halmashauri Kuu aliwaeleza juu ya
kuona umuhimu wa
kuanzisha zao hilo ni kutokana na kuona
kwa muda mrefu
watu wamekuwa wakikosa
chakula na kipato kutokana
nakutovuna kwa wingi
mazao kama mahindi
na mihogo ambayo
walikuwa wakilima.
Hata
hivyo alisema kuwa
zao la alizeti kwasasa
ndilo zao la uchumi katika wilaya ya
korogwe ambapo aliwataka
wakazi wa maeneo
hayo kulithamini na kulitunza
ili liweze kuwakomboa
kiuchumi na kuwapatia
kipato kikubwa.
Mndolwa
alieleza kama vijana
wataandaa mashamba hayo
ataweza kuwasaidia katika
kila kata kuwapatia
250,000 za kuanzia ili wafanye
shamba darasa na
hatimaye zao hilo
kushamili katika jamii nzima.
“
jamani vijana andaeni
maaeneo ya mashamba
ya ekali tano ili
tuweze kuanza kulima
alizeti kama mfano
wa zao hilo
ambalo hapo awali lilikuwa
halilimwi hapa korogwe”
Alisema Dk Mndolwa.

EmoticonEmoticon