HAJI JUMA KUZICHAPA NA MZUNGU WA ZANZIBAR PAMBANO LA KUWANIA UBINGWA WA TANZANIA (TPBO)

December 22, 2013
Na Oscar Assenga,Tanga.
BONDIA Haji Juma wa Tanga anatarajiwa kupanda ulingoni kuzichapa na Mohamed Mzungu wa Zanzibar katika pambano la kuwania Ubingwa wa Tanzania (TPBO) kg 52 superfly la raundi 10 litakaofanyika Desemba 25 mwaka huu kwenye uwanja wa Tangamano jijini Tanga.
Mratibu wa Pambano hilo, Promota Ally Mwazoa alisema pambano hilo linatarajiwa kuwa la aina yake kutokana maandalizi yaliyofanywa na uwezo walionao mabondia hao.
Mwazoa aliyataja mapambano ya utangulizi kuwa ni bondia Rajabu Mahoja na Jumanne Mohamed wote kutoka mkoani Tanga wataonyeshana kazi pambano la raundi 10 lenye uzito wa kg 57 feith weight.
Licha ya kuwepo pambano hilo mabondia wengine watakaozichapa ni Hamisi Mwakinyo wa Tanga atapambana na Said Mundi litakalokuwa la uzito wa kg 59 super feather raundi 6 huku Saimon Zabron naye atapigana na Athumani Boxers pambalo litakalo kuwa na uzito wa kg 61 Light weight raundi sita.
Mratibu huyo alisema pambalo lengine litakalo hitimisha raundi sita ni bondia J.J Ngotiko wa Tanga ambaye atapanda ulingoni kuzichapa na Zuberi Kitandula litakalokuwa la raundi sita super bantam.
Aliyataja mapambano ya mwisho siku hiyo yatakuwa na raundi nne nne ambapo bondia Jacob Maganga atazichapa na Mohamed Kidari pambano lenye uzito wa kg 65 light walter raundi nne wakati Juma Mustapha atapambana na Selemani Hamza litakalokuwa la raundi nne lenye uzito wa kg 55 super bantam.
Mratibu huyo alisema siku ya mapambano hayo,mgeni rasmi anatarajiwa kuwa msanii nguli wa filamu hapa nchini King Majuto.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »