KARETI PEMBA WAWEKA MIKAKATI YA MCHEZO HUO.

November 07, 2013
Na Masanja Mabula -Pemba .07/11/2013.
Wadau wa mchezo wa Kareti Wilaya  ya Wete ,  wameweka bayana mbinu na mikakati ya kuimarisha mchezo huo ili uweze kusaidia kupatiakana kwa ajira kwa vijana na kupunguza tatizo ka vijana kutegemea ajira kutoka Serikalini .

Wakizungumza kwenye kikao cha kujadili mbinu na mikakati ya kuimarisha mchezo huo , uliofanyika kwenye ukumbi wa Jamhuri , wamesema kuwa moja ya mikakati hiyo ni kuweka viwanja sehemu za wazi ili kuwafanya vijana wengi kujiunga na mchezo huo .

Kikao hicho ambacho kiliwashirikisha makatibu na wenyeviti wa vikundi vya kareti Wilaya hiyo , ambao walipitisha azimio la kufanya bonanza la mchezo huo ili kuitangaza na kuihamasisha jamii kutambua umuhimu wa mchezo huo .

Afisa Michezo Wilaya hiyo Suleiman Shavuai , akizungumza kwenye kikao hicho amewataka walimu wa mchezo wa karati Wilayani humo , kutafuta maeneo ya wazi na kuacha kufanya mazoezi sehemu za msituni jambo ambalo linawafanya vijan wengi kushindwa kujiunga na mchezo huo .

Amesema kuwa mchezo wa karati unaweza kuiletea sifa nchi , endapo vijana watakuwa tayari kujiunga , huku pia alitoa wito kwa wafadhili kujitokeza kudhamini mchezo huo .

Akizungumza kwa niaba ya wenzake katibu wa kikundi cha Scopion karate gruop cha Ole , ameitaka jamii kuelewa kwamba mchezo huo ni kama ilivyomichezo mingine , na kuwataka vijana kujiunga kwa wingi kwa ajili ya kujenga miili pamoja na kujipatia ajira .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »