Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(mbele katika Jukwaa)
akipokea Saalam ya heshima na Utii kutoka kwa Gadi Maalum ya Gwaride
lililoandaliwa na Wahitimu 72 wa Mafunzo Maalum ya Udereva katika Chuo
cha Magereza cha Ufundi na Udereva Kingolwira, kilichopo Mkoani
Morogoro. Hafla fupi ya ufungaji Mafunzo hayo imefanyika leo Novemba 1,
2013 katika viwanja vya Kingolwira, Morogoro.
Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja (kulia) akikagua Gadi
Maalum ya Gwaride lililoandaliwa Maalum kwa ajili ya Ufungaji Mafunzo ya
Udereva Kozi No. 19 ya Mwaka 2013 ambayo yamefanyika leo Novemba 1,
2013 katika Chuo cha Magereza cha Ufundi na Udereva Kingolwira, Mkoani
Morogoro.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja akimkabidhi cheti mmoja
wa Wahitimu wa Kozi ya Udereva, Cpl. Nuru kutoka Chuo cha Maafisa
Magereza Ukonga, Dar es Salaam. Cpl. Nuru ni minongoni mwa askari 11 wa
Kike ambao wamehitimu mafunzo Maalum ya Udereva leo Novemba 1, 2013 na
Mafunzo hayo yamefanyika kwa muda wa Mwezi mmoja katika Chuo cha Ufundi
na Udereva Kingolwira, Mkoani Morogoro ambapo jumla ya Askari 72
wamehitimu Mafunzo hao kwa ustadi mkubwa.