UWAWATA WAUNDA KAMATI YA WAJUMBE 10.

November 02, 2013
Na Oscar Assenga,Tanga
UMOJA   wa  waganga   na wakunga wa jadi Tanzania (UWAWATA)  umeunda kamati ya wajumbe 10 watakaoshughulika tatizo la uharibifu ikiwemo  kukomesha mauaji  kama vile ya Maalbino  na vikongwe nchini.
 
Aidha Umoja huo uliwaagiza waganga  na wakunga  wa tiba asilia nchini kujisajili kwenye umoja huo  na kuacha kufanya shughuli zao kibiashara na kwamba kazi ya tiba ni huduma na siyo biashara.
 
Akitangaza msimamo huo, kwenye mkutano mkuu  wa Mkoa uliyofanyika jana kwenye ukumbi wa  Sahare way  jijini hapa, Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja  huo, Dk  Rashid  Tengeza alisema kuwa  Uwawata  inajukumu la kuhakikisha matendo ya kikatili na kishirikina yanakoma na kuifanya jamii na taifa kuwa na amani.
 
Kwamujibu wa  Dk Tengeza  ambaye pia aliongozana na Katibu Mkuu wa taifa  wa Umoja huo, Dk  Daud  Nyaki  ni kwamba chanzo cha  mitafaruku,uchochezi na mauaji ni  ramli chonganishi zinazopigwa  na  waganga  wa tiba asilia wasiyowaaminifu.
 
“Sisi waganga  wa tiba asili ndiyo wenye jukumu la kulipoza taifa hili na kuwa la amani kwani majanga yanayotokea ni waganga wa tiba asilia wasiyowaaminifu kujihusisha na matendo  kama vile uchochezi,mitafaruku na mauaji” alisisitiza Dk  Tengeza.
 
Alisema ufike wakati waganga kudhibitiana wenyewe kwa wenyewe  na kwamba serikali inatarajia kuona matunda ya Umoja huo ikiwa ni kukomesha mauaji ya vikongwe na albino ambayo hufanywa ama kuchochewa na  wachawi  ama waganga matapeli.
 
Aidha  alisema chini ya Umoja huo waganga ni wawe  kiungo kati ya serikali na wananchi ambao ni wateja wao na kufichua kila uovu unaofanyika kwenye maeneo yao  na kubainisha kuwa kila mganga atakaefanya hivyo Umoja huo utakuwa mtetezi wake anapopata matatizo anapotoa tiba kwa wananchi.
 
Katika mkutano huo uongozi wa  UWAWATA  Mkoa ulijaza nafasi za wajumbe zilizokuwa wazi  ndani  ya kamati ya utendaji  ambapo mbali na Mwenyekiti wa Mkoa, Allan Nkong’ota, makamu mwenyekiti Bakari Mwinjuma. Katibu wa Mkoa ni  Omari Sinde na Zaina  Mkama msaidizi wake.
 
Hata hivyo katika uchaguzi huo uliyosimamiwa na Dk Nyaki  iliundwa pia kamati maalumu ya Mkoa  yenye watu kumi na kupewa jukumu la kufichua uharifu, kukomesha waganga matapeli, rambaramba,wapiga ramli chonganishi, mauaji ya albino na vikongwe.
 
Waliyochaguliwa kwenye kamati hiyo ambayo ilishirikisha wataalamu  kutoka taasisi mbalimbali nje ya Umoja huo, ni mwenyekiti wa kamati, Juma Lukuwa, (mganga) katibu ni Dege Masoli ambaye ni mwandishi wa habari mkoani hapa
 
Aidha wajumbe ni Abdalla Hamissi,Swalehe Shamsham,Mayasa Jabu,Mwajuma Bakari,Teresia Basilio,Mavumba Zuberi,Kulthumu Hussein akiwemo na mwandishi wa habari Elizabeth Kilindi.
 
Mwisho

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »