Timu
za Taifa za Future Taifa Stars na Taifa Stars zinacheza kesho (Novemba
13 mwaka huu). Mechi hiyo ya kirafiki itafanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya
Karume jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Mechi
hiyo ni maalumu kwa Benchi la Ufundi la Taifa Stars linaloongozwa na
Kim Poulsen kuangalia wachezaji kumi kutoka Future Taifa Stars
watakaoongezwa katika Taifa Stars tayari kwa mechi ya kirafiki ya
kimataifa itakayochezwa Novemba 19 mwaka huu jijini Arusha.
Watazamaji 300 tu wataruhusiwa kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 5,000.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imeingia kambini leo
(Novemba 12 mwaka huu). Miongoni mwa wachezaji wanaotarajia kuripoti ni
kipa Ivo Mapunda wa Gor Mahia.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

EmoticonEmoticon