DIWANI AMKINGIA KIFUA MTENDAJI WA KIJIJI.

November 15, 2013
Na Oscar Assenga,Mkinga.
DIWANI wa Kata ya Gombero wilayani Mkinga mkoani Tanga,Mohamed Bamba amewataka wananchi wa Kijiji cha Kichangani kuwa watulivu ikiwemo kushiriki katika shughuli za kimaendeleo wakati mchakato wa kurejeshwa fedha za serikali ya kijiji hicho 515,000 zilizopotea ukifanyika.

Bamba alitoa kauli hiyo jana wakati wa mkutano mkuu wa kijiji hicho
ambapo pamoja na mambo mengine ulikuwa ni kusoma mapato na matumizi kwa wananchi hao.

Wakiwa kikao hapo wananchi walihoji upotevu wa fedha hizo za serikali
ya kijiji hicho ambazo zilipotea kutokana na matumizi mabaya kwa kumtuhumu mtendaji wa kijiji hicho Hamisi Juma kuhusika na tuhuma hizo kwa kumtaka kuzirejesha haraka iwezekanavyo kabla ya kuchukuliwa hatua.

Akizungumza katika mkutano huo,mkazi wa kijiji hicho mchungaji Daudi
Malulu alisema suala la kiongozi huyo wa kijiji kufanya ubadhirifu wa fedha hizo ndani ya serikali utaweza kuwagawa wananchi ikiwemo kukwamisha maendeleo ya wananchi hivyo kuwataka viongozi hao kuwajibika kwa kuzilipa fedha hizo.
  “Ninaweza kusema suala hili sio la kufumbiwa macho tunaziomba
mamlaka husika kulivalia njuga ili kuweza kupatikana ufumbuzi wake kwani hali hiyo ikiendelea hivyo itapelekea kukwamisha miradi ya maendeleo “Alisema Malulu.

Naye mkazi wa kijiji hicho,Mzee Abdallah Mohamed Nzibo alitaka hatua
zichukuliwa dhidi ya mtendaji huyo kutokana na ubadhirifu za fedha za serikali ya kijiji hicho ili kuweza kuwa fundisho kwa watendaji wengine wenye tabia kama hizo.
 
Baada ya tuhuma hizo,Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Hamisi Juma
alisema suala la ubadhirifu wa fedha hizo alipokea na kuhaiadi
kulifanyia kazi ili waweze kupata majibu yake kwenye mkutano mkuu wa kijiji hicho utakaofanyika mwezi desemba mwaka huu.

Hata hivyo diwani Bamba alitolea ufafanuzi kuhusu tuhuma za mtendaji
  huyo za upotezo wa fedha hizo kwa kusema suala la sh.208000 zinajulikana na wapi zilipotea na watafuatilia ili ziweza kupatikana haraka iwezekanavyo.

Bamba alisema suala la 314000 wananchi pamoja na serikali ya kijiji
watakaa ili kuweza kufahamu fedha hizo zimepotea kwa nani ili ziweza kupatikana ili ulipwaji wake ufanyike haraka.

Hata hivyo diwani huyo alisisitiza upotevu wa fedha halali ambazo

zimepotea katika serikali ya kijiji hicho ni sh.208000 ambazo
watahakikisha wanafanya jitihada za kubaini muhusika wake ili
atakapobainika hatua kali za kisheria zidi yake ziweze kuchukuliwa.

Aliongeza kuwa fedha nyengine ambazo wameelezwa na wananchi wao
watahakikisha wanaziangalia kwa umakini katika mahesabu kwa sababu huenda zikawa zimekosewa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »