Na Masanja Mabula -Pemba .
Uongozi
wa klabu ya Coastal Union ya Tanga umewakata maini mashabiki wa timu
ya Jamhuri juu ya usajili wa wachezaji wake Abdalla Othman na Suleiman
Kassim Selembe wakati wa dirisha dogo na kusema kuwa wachezaji hao
wataendelea kuitumikia klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya Vodacom .
Mwenyekiti
wa klabu hiyo Hemed Aurora ameliambia blog hii kuwa taarifa za wachezaji hao kudaiwa kujiunga na timu ya Jamhuri kwa
mkopo wakati wa dirisha dogo hazina ukweli na kuongeza kwamba wachezaji
hao ni muhimu na wanawahitaji katika mzunguko wa pili ya ligi hiyo .
Amesema
kuwa wachezaji hao bado ni muhimu kwenye kikosi cha timu hiyo , na
kwamba mpango wa kuwatoa kwa mkopo haupo na badala yake
wanaangalia kuongeza wachezaji kuziba mapengo yaliyojitokeza katika
msunguko wa kwanza ulimalizika wiki hii .
"Taarifa
hizo hazipo kwenye klabu yetu , tunajua wachezaji hawa ni muhimu na
bado tunawahitaji , hivyo mpango wa kuwatoa kwa mkopo haupo na lwa sasa
tunaangalia mbele kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kwenye msunguko
wa kwanza " alieleza .
Aidha
amefahamisha kuwa kamati Tendaji ya klabu hiyo inatarajia kufanya kikao
mwishoni mwa wiki hii , ambapo ajenda itakuwa ni kujadili mwenendo wa
timu kwenye ligi kuu pamoja na kupitisha jina la kocha atakayechukua
nafasi iliyoachwa wazi na Hemed Moroco .
"Tumepokea
maombi ya makocha wanne , ambapo kati yao wawili kutoka nje ya nchi na
wawili ni wazalendo , kamati tendaji itakutana na kupitia vielelezo
vyao
ili kupata kocha atakayeiongoza timu kwenye duru la pili la ligi hapo
mwakani " alifahamisha .
Kabla
ya hapo kulikuwepo na taarifa ambazo zinawahusu wachezaji hao kujiunga
na Timu ya Jamhuri wakati wa dirisha dogo la usajili ili kuiongezea
nguvu timu hiyo ambayo ushiriki wake kwenye ligi kuu ya Zanzibar ni wa
kusuasua .
Taarifa
hizo zitazidisha machungu kwa mashabiki wa timu wa timu ya Jamhuri
ambao walikuwa wameanza kushusha presha kuwa timu yao imepata wachezaji
ambao watasaidia kuinasua na wimbi la kushuka daraja .
"Taarifa
hizi zimezidi kutuumiza kwani tulikuwa na furaha kwamba wachezaji hao
wawili wangetua kikosi cha timu yetu kingekuwa kimeiimarika " alisema
shabiki wakati alipozungumza na mwandishi wa habari hizi .
Timu ya Jamhuri ndiyo inayoshika mkia wa ligi kuu ya Zanzibar kwa kuwa na alama tatu baada ya kushuka uwanjani mara 11 .
EmoticonEmoticon