WASHABIKI WENYE SILAHA MARUFUKU VIWANJANI

October 04, 2013
NA BONIFACE WAMBURA,DAR ES SALAAM.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia Jeshi la Polisi kuanzia sasa halitashikilia silaha za washabiki, na badala yake litawazuia kabisa kuingia viwanjani wakati wa mechi.

Jeshi la Polisi limekuwa likihifadhi silaha za washabiki wanaokwenda viwanjani, na baadaye kuwarejeshea baada ya mechi kumalizika kwa vile Kanuni za Usalama Viwanjani za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) zinakataza silaha viwanjani.

Wikiendi iliyopita katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jeshi la Polisi lilikamata bastola 17 katika upekuzi wa washabiki waliokwenda kushuhudia mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting na ile kati ya JKT Ruvu na Simba. Wote waliokutwa na silaha hizo walikuwa na leseni za kuzimiliki.

Hivyo, kwa washabiki wanaomiliki silaha hatawaruhusiwa kabisa kuingia viwanjani, na badala yake tunawashauri kuzihifadhi huko wanakotoka kabla ya kufika viwanjani.

Pia tunatoa mwito kwa shabiki ambaye atamuona mwenzake akiwa na silaha uwanja kutoa taarifa kwa mamlaka husika likiwemo Jeshi la Polisi ili aweze kuchukuliwa hatua.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »