WAZIRI akataa kupokea mradi wa Maji wa zaidia ya Milioni 400 jimboni kwake.

July 19, 2013
Na Mwandishi Wetu,Bumbuli
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ambae pia ni Mbunge wa Bumbuli January Makamba amekata kupokea mradi wa maji wa zaidi ya Sh Mil 400 ambao ungehudumia vijiji vinne vilivyoko kwenye Jimbo la Bumbuli kutoka na kujengwa chini ya kiwango.

Hayo aliyasema wakati akiongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kiwanja cha stendi jimboni humo,alisema licha ya mradi huo kutengewa fedha nyingi na wahisani lakini haukutekeleza vile ulivyotakiwa.

Alisema mradi huo ulikuwa uanze kutoa huduma zake kuanzi kijiji cha Kwamanolo ambao ulikuwa ujenzi unaanzia pamoja na kujenga tanki lenye uwezo wa kuchukuwa lita lakimoja na thelathini na tano lakini tanki lilijengwa linachukuwa lita 90 tu

“Nimekata kuupokea mradi wa maji katika Jimbo langu kutoka na kutoridhishwa na ujenzi wake lakini pia nimemuomba waziri wa Maji Jumanne Maghembe atusaidi kuingiza kijiji kimoja katika mradi wa maji uofadhiliwa na Benki ya dunia wa kuhudumia vijiji kumi ili kupunguza shida ya maji Bumbuli”alisema Makamba.

Nae Diwani wa kata ya Bumbuli Tulo Guga alisema kuwa mradi huo ulikuwa unufaishe vijiji vya Bumbuli Mission,Bumbuli Kaya,Mboki na Kwamanolo lakini makubaliano ilikuwa kule eneo mradi unapoanzia nilazima maji yaanze kupatika na pamoja na ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji.

Aliongeza kuwa yote hayo mkandarasi hakuyatekeleza licha ya kazi ya ujenzi kukamilika kwa wakati ,lakini kikubwa zaidi ni kujenga tanki ndogo la kuhifadhia maji ambalo halitaweza kuhudumia wananchi wengi kwa wakati mmoja.

Hivyo aliiomba Halimashauri ya Wilaya ya Lushoto kuupokea mradi huo na kujaribu kurekebisha mapungufu kabla ya kuukabidhi tena kwenye Hlamshauri ya Bumbuli ili wananchi waweze kunufaika na mradi huo na kuondokana na kero ya maji .
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »