Kuachwa Kaseja na Simba ni Jambo la kawaida-Msumari

July 13, 2013
Na Oscar Assenga,Tanga.
WANACHAMA wa Simba Mkoa wa Tanga wamesema kuachwa kwa mlinda mlango Juma Kaseja kwenye
kikosi hicho msimu huu ni jambo la kawaida ambalo linaweza kumkuta mchezaji yoyote katika medani ya soka hapa nchini.

Akizungumza blog hii,Mwenyekiti wa Matawi hayo Mkoa wa Tanga,Mbwana Msumari alisema anashangaa kuibuka maneno mengi baada ya mlinda mlango huyo kuachwa na klabu hiyo msimu huu.

Msumari alisema wanachama wa timu hiyo na wadau waliibuka na maneno mengi ambapo kila kundi lilikuja na mtazamo wake kuhusu kuachwa kwa mchezaji huyo wengine wakidai itakuwa ni pengo kubwa kwa wasifu ya walinda milango ndani ya klabu hiyo,wengine wakidiriki hata kuandamana.

Alisema wakumbuke kwamba Kaseja huyo huyo aliwahi kutoka akaenda Yanga na Simba walicheza Ligi Kuu bila matatizo yoyote na kufanya vizuri bila kuwepo mlinda mlango huyo sasa anashangazwa na watu hao.

Aidha alisema ni lazima watanzania waache usajili wa mazoea ambao unaleta athari mara kwa mara kwa timu kwani Athumani Chuji aliwahi kuachwa na Yanga akaenda Simba na Yanga wakafanya vizuri kwa hiyo mabadiliko yanapokuja kwenye soka yasizuiliwe yaachiwe kocha afanye maamuzi yake.

Msumari alisema ni vizuri maamuzi ya Kocha yasiingiliwe kwenye maamuzi yao waachwe hao ni kamati ya usajili wafanye kazi yao  na hata makocha wa timu za ulaya wanafanya mabadiliko kutoka timu moja kwenda timu nyengine.

Hata hivyo aliongeza kwa Simba la ajabu ni lipi hapo alihoji Mwenyekiti huyo huku akisisitiza maamuzi yaliyofanywa na kamati ya usajili pamoja na kocha ni sahihi yaheshimiwe kwa maslahi ya timu inawezekana wameamua kwa sababu zao ambazo sie hatuzijui na hatuwezi kuhoji.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »