VETERAN SC yaanza vema Kombe la Takukuru Cup.

June 24, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
TIMU ya Veteran leo imeanza vema mashindano ya ligi ndogo ya Takukuru Cup baada ya kuilaza Makorora Star mabao 4-2 katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo mchezo uliochezwa uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Mchezo huo ulikuwa mkali na wa kusisimua kutokana na timu zote kuonekana kucheza kwa kukamiana ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko timu ya Makorora Stars ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-1.

Mabao ya Makorora Star yakifungwa na Hussein Salim ambaye alifunga mabao mawili kwenye dakika ya 6 na 45
Huku bao la Veteran FC la kwanza likipatikana kwenye dakika ya 9 kupitia Sadiq Rashid ambaye alitumia uzembe wa mabeki kupachika wavuni bao hilo.



Kipindi chaa pili kilianza kwa kasi kwa kila timu kuingia uwanjani hapo ikiwa na hari na nguvu mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ambapo, Veteran Sc walionekana kujipanga na kutaka kulipa kisasi.

Wakicheza kwa kusikilizana Veteran Sc waliweza kuongeza bao la pili ambalo lilifungwa na Tinath Tsungi katika dakika ya 55 huku Anderson Solomoni akiipatia timu hiyo bao la pili ambalo lilipatikana kwenye dakika ya 58 kwa njia ya penati.

Baada ya kuingia mabao hayo,Veteran waliweza kuongeza kasi ya mashambulizi langoni mwa Makorora na kufanikiwa kuandika bao lao la nne kupitia Faridini Hemed dakika ya 84 ambalo lilihitimisha karamu ya mabao kwenye mchezo huo.




Mashindano hayo yamefunguliwa leo na Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Tanga ,Edson Makallo na yanashirikisha timu 4 ambazo ni Makorora Star,Magomeni Sc,Bomboka Sc na Veteran yenye lengo la kuhamasisha mapambano dhidi ya rushwa kupitia michezo mkoani Tanga.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »