SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA SEKTA YA ELIMU KUPITIA MAFUNZO ENDELEVU

July 29, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imefungua mafunzo ya siku tatu ya Uongozi na Usimamizi wa Shule pamoja na Utawala Bora wa Elimu kwa Maafisa Elimu kutoka mikoa yote 26 na Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara yakiwa na lengo la kuongeza ufanisi na kuimarisha usimamizi wa sekta ya elimu nchini.

Waziri Kikwete aipongeza CRDB Bank Foundation kukuza ujasiriamali nchini

July 29, 2025 Add Comment

 

Kutokana na fursa zinazotolewa kwa wananchi kupitia Programu ya Imbeju, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete ameipongeza Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kukuza ujasiriamali na kuongeza elimu ya fedha kwa wananchi wengi zaidi.

Waziri Kikwete ametoa pongezi hizo kwenye uzinduzi wa shirika lisilo la kiserikali linalohamasisha ujasiriamali miongoni mwa vijana la National Enterprise Development Chamber (NEDC) uliofanyika mwishoni mwa wiki.
“Taasisi ya CRDB Bank Foudation mnafanya kazi kubwa sana katika kuwainua vijana kupitia Programu yenu ya Imbeju. Mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha mnayoitoa. Kujitoa kwenu kuilea NEDC nalo ni jambo muhimu litakalosaidia kuwajumuisha vijana wengi kwenye huduma rasmi za fedha,” amesema Waziri Kikwete.

CRDB Bank Foundation imedhamini uzinduzi wa NEDC inayoziunganisha biashara changa hasa za kibunifu ambazo nyingi zinamilikiwa na vijana, kuwaunganisha wafanyabiashara, wawekezaji pamoja na taasisi za umma ili kujenga ushirikiano utakaoboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, malengo ambayo ni miongoni mwa vipaumbele tunavyotekeleza CRDB Bank Foundation.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema wanashirikiana na kila mdau kuboresha maisha ya watu kutoka jamii zilizotengwa kifedha na kiuchumi kwa kutoa mafunzo ya ujasiriamali, elimu ya fedha na kuwapa mitaji wezeshi wajasiriamali wanaokidhi vigezo.

“Katika kuhamasisha maendeleo ya ujasiriamali na ubunifu, tunachochea ukuaji wa ubunifu na biashara changa za vijana, tunawawezesha vijana na wanawake kupitia mafunzo ya stadi za elimu ya fedha, ujasiriamali, usimamizi wa biashara, utunzaji wa kumbukumbu na mbinu za upatikanaji wa rasilimali fedha pamoja na Kuchochea ubunifu kupitia programu za kukuza na kuendeleza biashara changa,” amesema Tully.

Ili kuwa na maisha bora, Tully amesema ni muhimu kwa wananchi hasa wa kipato cha chini kujengewa wa kifedha , kukuza utamaduni wa kuweka akiba na uwekezaji pamoja na kuwajumuisha katika huduma rasmi za fedha vijana na wanawake bila masharti magumu.
“CRDB Bank Foundation (CBF) inatambua nguvu ya ushirikiano wa kimkakati katika kuleta mabadiliko chanya kwani ndio njia ya uhakika ya kufungua fursa zaidi kwa vijana na wanawake wajasiriamali nchini. Tunashirikiana na serikali kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kukuza suluhisho bunifu na tunashirikiana na sekta binafsi kuongeza uwekezaji katika ujasiriamali na elimu ya fedha,” amesema Tully.

Kwa upande wake, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji tena National Enterprise Development Chamber (NEDC), Jesse Madauda amesema wataendelea kushirikiana na serikali, taasisi za umma na binafsi pamoja na wabia wengine wanaopenda kumwinua Mtanzania kiuchumi.
“Kwa kuunganisha nguvu, rasilimali na mikakati, tunaamini tunaweza kuharakisha ukuaji wa biashara changa zenye uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko katika jamii,” amesema Madauda.

Benki ya CRDB yapongezwa kuwapa elimu ya ujasiriamali wajasiriamali wa mtandaoni

July 29, 2025 Add Comment

 


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Mheshimiwa Albert Chalamila ameipongeza Benki ya CRDB kwa jitihada zake za kuwaelimisha wajasiriamali wa mtandaoni kuhusu fursa zilizopo na namna wanavyoweza kushirikiana na taasisi hii kubwa zaidi ya fedha nchini kujikwamua kiuchumi.

Pongeza hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki kwenye Semina ya Instaprenyua iliyowakutanisha wajasiriamali na waelimishaji wa mada tofauti kuhusiana na jinsi wanavyoweza kukuza biashara zao na kujiongezea kipato.

Akizungumza na wajasiriamali hao, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Charangwe Makwiro aliyemwakilisha Mheshimiwa Chalamila amesema kinachofanywa na benki ya CRDB kuwajengea uwezo wajasiriamali kinaunga mkono jitihada za serikali inayojitahidi uweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji nchini kukuza kipato chao.

“Maarifa ya kufanya biashara ni nyenzo muhimu ya mafanikio katika biashara pengine kuliko hata mtaji fedha. Mafunzo haya yanayotolewa na Benki ya CRDB yanafungua fursa ambazo mjasiriamali hakuwa anazifahamu. Nawapongeza sana Benki ya CRDB kwa kutenga muda wa kukaa na wajasiriamali hawa na kuwaonyesha namna ya kushirikiana nanyi kukuza biashara zao,” amesema Charangwe.

Kukua kwa sayansi na teknolojia kumerahisisha mambo mengi duniani katika karne hii ya 21 ikiwamo namna ya kufanya biashara kwani sasa hivi kwani mfanyabiashara anaweza kumuuzia mteja ambaye haaonani na kila kitu kikaenda vizuri.

Charangwe amesema Serikali imeweka juhudi kubwa kuhakikisha Watanzania wananufaika na fursa zilizopo kwenye mitandao ya kijamii kwa kuweka mazingira rafiki ya kumiliki simu za kisasa, upatikanaji wa intaneti pamoja na ulinzi wa taarifa za watumiaji wa mitandao ya kijamii.

“Takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonyesha mpaka Juni 2025 tulikuwa na jumla ya laini milioni 92.7 za simu zilizosajiliwa na kati ya hizi, zaidi ya laini milioni 54.1 zilikuwa zinatumia intaneti. Idadi ya watu waliofikiwa na huduma za intaneti ni asilimia 93. Ongezeko la matumizi ya intaneti nchini linatokana na kukua kwa mahitaji. Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara ikiwamo kujenga miundombinu ya mawasiliano,” amesema Makwiro.

Akieleza kuhusu mikakati ya kuwawezesha wajasiriamali nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema Semina ya Instaprenyua ni jukwaa mahsusi la kujadili teknolojia mpya, mbinu bunifu za masoko, ulinzi wa kidijitali, na jinsi wajasiriamali wa mtandaoni wanavyoweza kunufaika na mikopo nafuu kutoka benki ya CRDB.

“Katika dunia ya leo ya karne ya 21, biashara si suala la mahali tena bali namna gani muuzaji anaweza kumfikia mteja. Hii ndiyo sababu Benki ya CRDB tumeendelea kuipa umuhimu mkubwa semina hii ya Instaprenyua tangu tulipoizindua mwaka 2022 tukitambua kwamba katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la matumizi ya teknolojia katika kuendesha biashara, jambo kubwa ambalo mjasiriamali wa kisasa hawezi kulikwepa,” amesema Nsekela.

Benki ya CRDB, amesema inamrahisishia mfanyabiashara kukusanya malipo anayoyapokea kupitia huduma ya LIPA HAPA kutoka kwa mteja hata aliye mbali naye huku ikimruhusu mteja kulipia bidhaa au huduma azitakazo SimBanking, mitandao ya simu, au TemboCard. Mifumo hii yote amesisitiza kuwa ni ya haraka, ina usalama na ufanisi mkubwa na ndiyo msingi wa biashara ya kidijitali yenye mafanikio.

Kuhusu upatikanaji wa mitaji, Nsekela amesema “Benki ya CRDB imekuwa kinara katika uwezeshaji wa wajasiriamali kupitia Akaunti ya Hodari ambayo ni kwa ajili ya wajasiriamali wadogo na Akaunti ya Biashara kwa wajasiriamali wa kati.
Akaunti hizi huwaunganisha wajasiriamali na fursa za mikopo ya uwekezaji na mikopo ya uendeshaji ikiwamo ‘Komboa loan’ mahsusi kwa wafanyabiashara wanaoagiza mizigo kutoka nje ya nchi. Vilevile tunatoa mitaji wezeshi kupitia Taasisi yetu ya CRDB Bank Foundation ambapo wafanyabiashara wachanga hupewa kwanza kabla hawajapewa mitaji wezeshi kukuza biashara zao.”