VERTEX YAJA NA UWEKEZAJI KIGANJANI

May 27, 2025 Add Comment



NA MWANDISHI WETU

MTENDAJI Mkuu wa Vertex International Securities limited Mateja Mgeta amewataka watu kuwekeza kupitia huduma ya Vertex Mobile Trading App ambayo itawasaidia wananchi kufanya uwekezaji kwa wepesi kwa kuwa ni moja ya njia nyepesi kwa watumiaji.

Mateja amebainisha hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Vertex Mobile Trading App yenye lengo la kuwapa wepesi wawekezaji kupitia simu janja zao.

Amesema lengo la ujio wa app hiyo una sura mbili ambazo ni kuwapa watu maarifa ya uwekezaji kwa urahisi iwe mtu anahitaji kuwekeza hisa katika makampuni yaliyoorodheshwa na soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) hivyo imani ni kubwa kuwa elimu ndio funguo ya ushiriki wa uwajibikaji.

Sababu ya pili iliyowasukuma kuanzisha Vertex Mobile Trading App kulenga kurahisisha mfumo wa uwekezaji kuufanya uwe wazi, rahisi na salama kwa watumiaji ambao mwekezaji au mwekezaji mtarajiwa anayetumia simu janja (smart phone) anaweza kufungua akaunti ya hisa, kununua au kuuza hisa kupitia kiganjani pasipokuwa na ulazima wa kufika ofisni kwao.

"Masoko ya mitaji yana jukumu muhimu sana katika kukusanya fedha kwa ajili ya matumizi yenye tija yanayotumika kama njia ambazo akiba inaweza kuelekezwa kwenywe miradi inayochochea ukuaji wa uchumi, ubunifu na kutengeneza ajira,"amesema Mateja.

Aidha Mateja amesema uwekezaji uchangia kikamilifu katika ajenda ya uchumi wa Taifa, hivyo kutokana na uwekezaji unaweza kuimalisha masoko ya mitaji ya ndani, kupunguza utegemezi wa ufadhili kutoka nje na kukuza uwekezaji utakaochochea ustawi wa pamoja.

Mateja ametoa pongezi kwa mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Tanzania (CMSA) chini ya Mtendaji wake Mkuu CPA Nicodemus Mkama kwa kuweka mazingira wezeshi katika soko kwani bila miongozo yao wasingeweza kufika walipo sasa.

Pia alitoa pongezi kwa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Peter Nalitolela kwa mchango wao mkubwa kuhakikisha Vertex Mobile Trading App mafanikio ya hisa kiganjani ambayo yamefanywa na wao Vertex International Securities limited.

Kwa upande wa mwakilishi kutoka CMSA Alfred Mkombo amesema wao mamlaka ya msoko ya mitaji wanafurahi kuona maendeleo kama haya ambayo yanawapa watu urahisi wa kuwekeza kupitia simu zao viganjani.

"Simu imekuwa kitu kikubwa zipo hadi vijijini mtu anaweza kushiriki minada inayotokea Dar es Salaam bila kusafiri na kutumia gharama kubwa, Vertex Mobile App imetengenezwa ili kuleta mageuzi na ni tekinolojia ambayo inatumika kwa wepesi bila hata kutumia nguvu,"

"Tunapenda kuona teknolojia hizi zinaleta tija zaidi tunawapongeza sana Vertex kwa namna ya kipekee kufikia hatua hii kubwa sana ya mafanikio ambayo inaakisi sera na sheria usimamizi unaoleta mazingira bora,"amesema Mkombo.

Huku Ali Othman kutoka DSE amesema jambo lililofanywa na Vertex ni kubwa na litaleta mafanikio makubwa kwa kuwa ni njia nzuri na rahisi kwa watu kutumia.

"App ina kila kitu kwa mtumiaji wa mtandao wowote Vertex Mobile Trading App imewarahisishia hii ni hatua nzuri inaongeza ushindani na ubunifu mpya kwa watu wote kuwekeza iwe mjini na hata vijini,"amesema Othman.









SERIKALI YAITAKA COMMUNITY NETWORK KUSAMBAZA TEHAMA VIJIJINI

May 27, 2025 Add Comment
Serikali kupitia Tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeitaka Taasisi ya School of Community Network kuongeza juhudi za kuanzisha vituo vya mafunzo ya TEHAMA katika mikoa mbalimbali nchini, hususan vijijini, ili kuwajengea vijana ujuzi wa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidigitali.

LESOTHO WAVUTIWA NA REA

May 27, 2025 Add Comment
-Wampongeza Rais Samia katika suala la uhamasishaji wa nishati safi ya kupikia

MBOGGO ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA TANGA KUPITIA ACT- WAZALENDO HUKU AKIHAIDI KUIREJESHA TANGA YA VIWANDA

May 27, 2025 Add Comment
Katibu wa Chama cha ACT -Wazalendo  Wa Jimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda (kushoto)  akimkabidhi fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Ubunge Jimbo la Tanga mwanachama wao John Charles Mboggo  (katikati)  kulia ni Mwenyekiti wa Wazee Jimbo la Tanga (ACT Wazalendo) Zaharan Mohamed


Na Oscar Assenga, Tanga.

KADA wa Chama Cha ACT –Wazalendo Mkoani Tanga John Charles Mboggo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania Ubunge katika Jimbo la Tanga kupitia chama hicho huku akihaidi kuirejesha Tanga ya Viwanda ambayo ni ndoto kubwa ya wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo alisema lenbgo la kuchukua fomu ya kuwania Ubunge ni kutaka kuhakikisha anatoa mchango wake katika kurejesha viwanda vya Tanga ambavyo wananchi wamekuwa na kiu navyo.

Alisema kwamba kwa sababu viwanda ni ajira  na nguvu kazi ya Tanga wanaongelea kuna vijana asilimia 68 ya vijana wakitumika kwenye viwanda watakuwa na uchumi kwenye Jimbo hilo na Mkoa kwa Ujumla.

“Tanga tunaamini sisi ni watu tunaamini watu wa kuleta maendeleo na ndio maana tunawahamasisha wananchi wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la kura  kwa lengo la kuwachaguoa viongozi watakaowaongoza”Alisema



Aidha alisema kwamba wasione aibu kutokana na uwepo wa hila mbalimbali wanajua namna ya kubaliana nayo ili kuhakikisha hazijitokezi kwenye mchakato huo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Jimbo la Tanga  Anasi Mohamed Rweymamu alisema kwamba wanaendelea kuwakaribisha wagombe na kura zao wa maoni ndani ya chama ndizo zitakazoamua nani anaweza kupeperusha tiketi ya chama hicho kwenye nafasi ya Ubunge.

Alisema kwamba ACT Wazalendo ndio chama pekee ambacho kinaweza kupeperusha vyema Bendera yake katika kuibuka na ushindi kwenye nafasi ya Ubunge Jimbo la Tanga na Tanzania kwa upekee.

Naye kwa upande Katibu wa ACT  WaaJimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda alisema kwamba wapo kwenye maandalizi ya uchaguzi kama chama hicho Taifa kilipotangaza kwamba zoezi la kuchukua fomu kutoka Aprili 18 mwaka huu mpaka 31 mwezi Mei katika nafasi za Ubunge na Udiwani.

Alisema kwamba katika uchaguzi huo wamejipanga kwamba wagombea watakao wapitisha katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo watakuwa imara kuhakikisha wanapeperusha vyema bendera hiyo.

Mwisho.

TPAWU YATAKA MCHAKATO KIMA CHA CHINI SEKTA BINAFSI UHARAKISHWE

May 27, 2025 Add Comment

 

 Mwenyekiti TPAWU Taifa Daniel Bariyanka Joachim akizungumza kwenye kikao hicho

Na Godwin Myovela, Morogoro

CHAMA cha Wafanyakazi Mashambani na Kilimo nchini (TPAWU) kupitia kikao cha Baraza Kuu la chama hichoTaifa, kimeomba kuharakishwa kwa mchakato unaoendelea wa kupanga kima cha chini cha mshahara sekta binafsi, kuzingatia maoni ya wadau-sambamba na kuhakikisha kima hicho kutopungua Tsh. 350,000 kwa mwezi, ili kusaidia kumudu gharama za maisha.

Mwenyekiti TPAWU Taifa, Daniel Joachim, alitoa tamko hilo wakati wa kikao hicho kilichofanyika mkoani hapa mwishoni mwa wiki, ambapo pamoja na mambo mengine, alieleza baraza hilo limezingatia hotuba ya Rais aliyotoa wakati wa kilele cha sherehe za Mei Mosi mwaka huu, kuhusu utaratibu wa kisheria unaoendelea kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.

“Kufuatia tamko la Rais mkoani Singida, tunamuomba waziri mwenye dhamana kuharakisha mchakato wa utafiti wa kima cha chini cha mshahara sekta binafsi na kitangazwe kwenye gazeti la serikali ili kianze kutumika sambamba na kile cha watumishi wa umma kitakachoanza Julai Mosi mwaka huu,” alisema Joachim  na kuongeza;

“Wakati wa mchakato huo baraza linamuomba waziri mwenye dhamana pamoja na bodi ya kima cha chini cha mshahara sekta binafsi ifanye maandalizi hayo kwa kuzingatia maoni ya wadau ambao ni waajiri na wafanyakazi.”

Aidha, baraza hilo limewaomba waajiri wote kuzingatia takwa la sheria la majadiliano mahali pa kazi ili kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia mikataba ya hali bora za kazi kwa mujibu wa kifungu cha 68 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini sura ya 366.

Katika hatua nyingine, Tpawu imekemea na kulaani vitendo vya baadhi ya waajiri ambao hutumia kima cha chini cha sekta husika kama sababu ya wao kutoongeza mishahara, jambo ambalo halikubaliki.

“Huu ni mtazamo potofu sababu unakwamisha lengo la kutungwa kwa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, pamoja na Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani Na. 98 vinavyotoa haki ya majadiliano mahali pa kazi,” alisisitiza Joachim

Hata hivyo, alimsihi Rais Samia kusaidia wafanyakazi wa sekta binafsi hasa sekta ya kilimo kupata mshahara unaoweza kuwasaidia kumudu gharama za maisha ya kila siku-mathalani-ikiwa sekta ya umma watalipwa kima cha chini Tsh.500,000 basi sekta binafsi kima cha chini kabisa kisipungue Tsh.350,000 kwa mwezi.Katibu Mkuu TPAWU Taifa John Vahaye akizungumza kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho

Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakifuatilia ajenda mbalimbali kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho