Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts
KATIBU MWENEZI CCM PAUL MAKONDA AHIMIZA WATANZANIA KUIPENDA NCHI YAO KWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

KATIBU MWENEZI CCM PAUL MAKONDA AHIMIZA WATANZANIA KUIPENDA NCHI YAO KWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

January 25, 2024 Add Comment






*Atoa rai kwa Watanzania kutotoa maneno ya kulaani Nchi kwani kufanya hivyo ni kujinyima mafanikio katika Nchi uishiyo._

“Tuna kila sababu ya kuipenda Tanzania, ndio nchi yetu, hazina yetu, urithi wetu na ndio mpango wa Mungu wetu kuwepo hapa lazima tuendelee kuimarisha Amani na Utulivu wetu”

“Watu wengi wanapenda kulaani nchi yao lakini mimi niwasihi isije ikatokea jambo ukaanza kutamka maneno ya laana kwasababu hautafanikiwa kwenye nchi uliyoilaani”

“Ukikasilishwa na mtu usitoe neno la kulaani Taifa lako kwakuwa Taifa hili ndio litabeba watoto wa watoto wako kama sio wewe basi watakula neema watoto zako na kama sio watoto zako basi wajukuu zako”

“Kwahiyo tuendelee kuliombea Taifa letu na Rais Samia na tunaposema tumuombee Rais wetu na Viongozi wetu watu wengi wanahitaji tunataka kuwaombea nini, we fikiria kama sio Utulivu, Msaada, Upendo wa Rais Dkt. Samia leo hii kungekuwa na maridhiano? na haya yote anaendelea kuyafanya kwa kuzingatia kanuni yake ya 4R ? Ndio maana tunasema tumuombee”

Makonda ameyasema hayo wakati akiwahutubia wana CCM na wanamchi wa Babati mkoani Manyara akiwa katika Diary yake ya kuhamasisha uhai wa Chama cha Mapinduzi na utlfuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi inayoendelea katika mikoa 20 ya Tanzania.

    

DK. NCHIMBI AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA ANC KOMREDI MBALULA

January 25, 2024 Add Comment

 

 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akipokea zawadi ya kitabu kiitwacho "Dare Not Linger: The Presidential Years" kilichoandikwa na aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela na Mandla Langa, kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Africa National Congress (ANC), chama tawala cha Afrika Kusini, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS),  leo Jumatano, Januari 24, 2024. 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa kwenye mazungumzo na Katibu Mkuu wa Chama cha Africa National Congress (ANC), chama tawala cha Afrika Kusini, Komredi Fikile Mbalula, ambaye yuko nchini kwa ajili ya kushiriki kikao cha Makatibu Wakuu wa Vyama Sita Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, kitakachofanyika Januari 25, 2024, nchini Tanzania. Mazungumzo ya makatibu wakuu hao wawili yamefanyika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS),  leo Jumatano, Januari 24, 2024.



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha Africa National Congress (ANC), chama tawala cha Afrika Kusini, Komredi Fikile Mbalula, leo Jumatano, Januari 24, 2024, walipokutana kwa ajili ya mazungumzo yaliyofanyika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha, mkoani Pwani.  




MWENEZI MAKONDA AAMKIA OFISI ZA HALMASHAURI JIJI LA ARUSHA

MWENEZI MAKONDA AAMKIA OFISI ZA HALMASHAURI JIJI LA ARUSHA

January 24, 2024 Add Comment

 

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amefika katika Ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Arusha kuona utekelezaji wa Agizo la Chama Cha Mapinduzi aliilotoa la kumtaka Mkuu wa Mkoa kuhakikisha Ofisi inafunguliwa na kusikiliza, kutatua na kusuluhisha migogoro, kero na changamoto mbalimbali za Wananchi.

Makonda amesema jambo hilo lisiwe la siku moja na isiwe kusubiria hadi viongozi wa kitaifa waje na watoa maagizo na badala yake wao wenyewe kujiwekea taratibu hizo ili kusudi kuhakikisha changamoto za Watanzania zinatatuliwa kwa wakati na kufikia dhamira ya Mwenyekiti wa CCM na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.