WIZARA YA MALIASILI YAZIDI KUWA TISHIO KWENYE MICHEZO YA KIRAFIKI KUELEKEA SHIMIWI 2024
michezo
RIADHA TANGA KUMPA USHIRIKIANO MUANDAAJI WA MASHINDANO YA TANGA CITY MARATHON
michezoMwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Tanga Sophia Wakati akizungumza
Na Oscar Assenga, Tanga.
CHAMA cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) kimesema kwamba kitampa ushirikiano wa kutosha muandaaji wa Mashindano ya Riadhaa ya Tanga City Marathon ili kuweza kuondoa changamoto zilizojitokeza msimu uliopita na yaweza kuwa na tija na mafanikio makubwa.
Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha (RT) Mkoa wa Tanga Sophia Wakati alipokuwa akizungumza na vyombo bya habari kuhusu namna walivyojipanga kuhakikisha wanampa ushirikiano wa kutosha muadaaji huyo ili mashindano hayo yaweze kufanyika kwa ufanisi.
Alisema pia kuweza kufanyika vizuri kwa kufuata taratibu zote za Mashindano hayo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kupitia Afisa Michezo Mkoa
“Mbio hizi za Tanga City Marathon ni mashindano muhimu kwa mchezo wa Riadha mkoani hapa na kwa sasa tumeyaingiza kwenye kalenda ya Mkoa na sasa yatakuwa yakifanyika kila mwaka na sisi RT kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa waandaaji”Alisema Sophia Wakati.
Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Septemba 22 mwaka huu ambapo yataanzia kwenye Hotel ya Tanga Beach Resort na kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia hapo huku yakishirikisha wakimbiaji katika makundi matatu ya Kilomita 21,10 na 5 za kujifurahisha.
HOME GUARD FC, SMALL PRISON ZAAGA MASHINDANO ULINZI CUP TANGA
habari michezoNa Oscar Assenga, TANGA.
TIMU za soka Small Prison na Home Guard zimeaga Mashindano ya Ulinzi Cup baada ya kila mmoja kufungwa katika mchezo wa hatua ya mtoano inayoendelea kwenye viwanja vya Ziwani Pongwe Jijini Tanga.
Mashindano hayo yanaratibiwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga yakiwa na lengo la kutoa elimu kwa vijana kujiepusha na vitendo vya uhalifu katika jamii wanazoishi ikiwemo kuwa mabalozi wa amani kwenye maeneo yao
Katika mchezo wa awali wa ufunguzi wa mashindano hayo timu ya soka TFC waliigaragaza Home Guard bao 1-0 bao ambalo lilifungwa na Mohamed Saidi dakika ya 5 hya mchezo huo ambao ulikuwa na upinzani.
Huku mchezo wa pili uliochezwa Agosti 21 mwaka huu timu ya Chote FC waliweza kuwapigisha kwata maafande wa Jeshi la Magereza Small Prison bao 1-0 ambalo lilifungwa na Boniface Majere dakika ya 47.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mashindano hayo,Diwani wa Kata ya Pongwe (CCM) Mbaraka Sadi alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuhakikisha Jeshi la Polisi linakuwa karibu na Jamii jambo ambalo ni muhimu katika kuhakikisha kuimarisha ulinzi.
Mbaraka alisema kwamba kufanyika kwa mashindano hayo katika maeneo mbalimbali yanasaidia na kuwawezesha vijana kuweza kuyatumia kama njia muhimu ya ajira,kujenga afya pamoja na kusaidia kuwaondoa vijana kwenye masuala ya uhalifu na dawa za kulevya na wanaamini mashindan hayo yatakuwa chachu kubwa ya kuinua vipaji vya wachezaji.
Naye kwa upande wake Mratibu wa Mashindano hayo Sophia Wakati alivitaka vilabu vinavyoshiriki kwenye mashindano hayo kuhakikisha wanazingatia sheria 17 za mpira wa miguuu zilizowekwa ikiwemo kuacha kuwachukia waamuzi.
“Lengo la Mashindano hayo ni kujenga undugu baina ya Jeshi la Polisi na Jamii lengo kujenga urafiki msijengeane chuki hakikisheni mnacheza kwa kuzingatia nidhamu ambayo itakuwa chachu ya mafanikio kwenye jambo lolote lile lakini msiwachukie waamuzi kutokana na kwamba wakati mwengine kunakuwa na makosa ya kibinadamu”Alisema
DKT.BITEKO APONGEZA JITIHADA ZA CRDB BANK MARATHON KUSAIDIA WATOTO, WAKINA MAMA NA VIJANA
habari michezo

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo wakati wa kilele cha msimu wa tano wa CRDB Bank Marathon ambapo Shilingi Milioni 350 zimekusanywa kwa ajili ya kusaidia watoto wenye uhitaji wa upasuaji wa moyo Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI), huduma za afya kwa wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT, na uwezeshaji wa vijana.

Akizungumza Waziri wa Sanaa, Utamaduni, na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema CRDB Bank Marathon imesaidia kwa kiasi kikubwa kuchochea ari ya michezo nchini. Dkt. Ndumbaro amesema mbio hizo zimekuwa jukwaa muhimu kwa wanariadha nchini kuonyesha vipaji vyao katika jukwaa la kimataifa kwani mbio hizo zimesajiliwa kimataifa na Shirikisho la Upimaji Mbio Kimataifa (AIMS) na Shirikisho la Riadha Duniani (World Athletic).
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema katika kiasi cha fedha kilichokusanywa; shilingi milioni 100 zitakwenda kusaidia watoto wenye uhitaji wa upasuaji wa moyo Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI), Shilingi Milioni 100 kusaidia huduma za afya kwa wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT, na Shilingi Milioni 150 uwezeshaji wa vijana.
Katika mbio hizo zawadi za jumla ya Shilingi Milioni 98.7 zimetolewa kwa washindi 60 wa mbio za kilometa 42, 21, 10, 5, pamoja na mbio za baiskeli za kilometa 65. Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank Foundation, Martin Warioba amesema jumla ya washiriki waliojiandikisha mwaka huu ni 8,000 huku akisema lengo la mwaka kesho ni kupata washiriki 10,000 Tanzania, huku malengo ya washiriki Burundi na DRC wakiwa ni 3,000 kila nchi.
Mbio hizi zilizofanyika Dar es Salaam ni za tatu baada ya zile zilizofanyika nchini DRC, na Burundi. Nchini DRC mbio hizo zilifanyika tarehe 4 Agosti ambapo Dola za Marekani 50,000 zilikusanywa kusaidia kuboresha huduma za afya kwa watoto hospitali ya Jason Sendwe jijini Lubumbashi. Kwa upande wa nchini Burundi, mbio hizo zilifanyika tarehe 11 Agosti ambapo Faranga za Burundi Milioni 120 zilikusanywa kusaidia wahanga wa mafuriko mkoa wa Gatumba jijini Bujumbura.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya mbio hizo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amewapongeza washindi wa mbio hizo, na kuwashukuru washirika wa mbio hizo wakiwemo kampuni za bima Sanlam na Alliance Life ambao ni washirika wakuu wa mbio hizo. “Tunawashukuru sana washirika wetu na wakimbiaji wote kwa kuungana nasi katika juhudi za kusambaza tabasamu kwa watoto walioathirika,” amesema Mwambapa.
Washindi wa mbio hizo Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Moses Nengichi kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Sara Makera kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Hamida Nasor kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Mao Hindo Ako kutoka Tanzania.
Sara Makera mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT.
“Mimi kama mwanamke ninajisikia faraja kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Watu wanapaswa kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoro na wakinamama pia hawastahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuunganisha pamoja katika juhudi hizi,” amesema.