Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. (Picha na INEC).
MWANASHERIA CHIPAMBA: KUJENGA JENGO BILA MIUNDOMBINU YA WALEMAVU FAINI NI MILIONI 20
habari
Mwanasheria Baraka Chipamba wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), akizungumza na watu wenye ulemavu kutoka Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB), Mkoa wa Dar es Salaam alipokuwa akitoa elimu kuhusu sheria ya watu wenye ulemavu Aprili 29, 2025.
.............................
Na Mwandishi
Wetu, Dar es Salaam
MWANASHERIA
Baraka Chipamba wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) amesema ni kosa kisheria kujenga jengo ambalo
halina miundombinu ya kuwasaidia watu wenye ulemavu na faini yake ni Sh.
Milioni 20.
Chipamba
aliyasema hayo Aprili 29, 2025 wakati akizungumza na watu wenye ulemavu kutoka
Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB), Mkoa wa Dar es Salaam alipokuwa akitoa elimu kuhusu sheria ya watu wenye
ulemavu mafunzo yaliyoratibiwa na LRCT na kufanyika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa
ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Alisema kosa hilo la kujenga jengo bila ya
kuwa na miundombinu ya watu wenye ulemavu likifanywa na Serikali faini yake ni
Sh. Milioni 2 na isizidi Milioni 20 na kama litafanywa na mtu binafsi ni faini
isiyopungua Sh. 500,000 hadi Sh.Milioni 7 au kifungo cha mwaka mmoja au vyote
kwa pamoja.
Alisema kwa mujibu wa sheria ya watu wenye ulemavu kama wananchi wengine wanayo haki ya kuheshimiwa, kutobaguliwa, kupata ajira, matunzo na stahiki zote wanazozipata watu wengine ikiwemo elimu.
“ Upo
umuhimu wa kuwepo vyama vya watu wenye ulemavu ili kuwakilisha na kujisemea
katika ngazi mbalimbali, kufanya utambuzi wa mahitaji yao pia kutathmini huduma
zinazotolewa na kuchochea maendeleo yao,” alisema Chipamba.
Alisema Serikali
ya Tanzania imeridhia au kuonesha nia ya kuwa sehemu ya juhudi za kimataifa ya
kuwainua na kuwalinda watu wenye ulemavu kwa kuwapatia fursa mbalimbali.
“Tunatambua
Tanzania imeridhia na kusaini Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu Wenye
Ulemavu (CRPD-2006 na Mkataba wa Nyongeza wa Haki za Watu Wenye Ulemavu 2009).
Lakini pia tunatambua kuwa kuna mambo mengi yamekwisha tekelezwa na Serikali,”
alisema Chipamba.
Mwanasheria
wa Tume hiyo, Vicky Mbunde ambaye alitoa elimu ya jinsi ya kuandika wosia na
kufungua shauri la mirathi alisema Watu wenye ulemavu wanayo haki na nafasi ya
kujiendeleza na kupata huduma katika jamii sawa na watu wasio na ulemavu.
Alisema ushiriki
wa watu wenye ulemavu katika maisha ya kila siku katika jamii hauna budi
kulenga katika kupunguza au kuondoa maisha ya utegemezi hivyo aliwahimiza
kufanya kazi kwa bidi kama vile ujasiriamali na shughuli zingine ili kujiletea
maendeleo yao badala ya kusubiri kusaidiwa.
Katika
mafunzo hayo mambo kadhaa yaliibuka ikiwa ni pamoja na jinsi wanavyoitwa ni ‘Watu
wenye Ulemavu au Walemavu’ ambao wanasheria wa Tume hiyo walieleza kuwa
wanatambulika kama ni Watu Wenye Ulemavu na siyo Walemavu.
Akichangia
mada kuhusu suala la kuandika wosia na mgawanyo wa mali zilizoachwa na marehemu
kwa wanufaika baada ya kufungua mirathi, Azamu Mohamed kutoka Yombo Dovya alisema
dini ya Kiislam haimtambui mtoto aliyezaliwa kwa mama mwingine nje ya ndoa
jambo ambalo linawafanya wanaume wengi kuwakataa watoto hao hivyo kushindwa
kupata mgao wa mali za baba zao pindi wanapofariki.
“Wanaume ule
ujasiri mliotumia wa kutoka kwa wake zenu na kwenda kuchepuka na kuwapata
watoto hao mnatakiwa kuuonesha kwa kuwatambulisha kwa wake zenu na ndugu ili
nao wajulikane na kupata mgao huo badala ya kuwakana,” alisema.
Mweka hazina
wa Jumuiya hiyo, Seif Jega, akizungumza baada ya kupata nafasi ya kushukuru kwa
niaba ya washiriki baada ya mafunzo hayo aliupongeza uongozi wa Tume hiyo kwa
kuandaa mafunzo hayo kwa watu wenye ulemavu na kuomba yawe endelevu ikiwa ni
pamoja na kuyafikisha vijijini wenzao na jamii waweze kuielewa jambo ambalo
litaweza kupunguza unyanyapaa kwa kundi hilo.
Kuhusu Tume hiyo, Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) ni Idara ya Serikali
inayojitegemea chini ya Wizara ya Katiba na Sheria ambayo imeanzishwa kwa
mujibu wa Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Sura ya 171, na
ilianza kazi rasmi tarehe 21 Oktoba, 1983.
Kwa mujibu wa sheria, Tume ina jukumu la kufanya mapitio ya sheria zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ziandane na mazingira ya wakati uliopo kwa maendeleo endelevu.
Mwanasheria Vicky Mbunde wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), akitoa elimu kuhusu namna ya kuandika Wosia pamoja na kufungua mirathi.Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Iddi Damka, akiongoza mafunzo hayo.
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Judika Magezi akizungumza.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Maswali yakiulizwa kutoka kwa washiriki wa mafunzo hao.
Asha Kinyama akichangia jambo kwenye mafunzo hayo
Maswali yakiendelea kuulizwa.
Margareth Mhina, akizungumzia umuhimu wa faragha wakati wa kumuhudumia mtu mwenye ulemavu anapokwenda kupata matibabu hospitalini.
Maswali zaidi yakiulizwa.
Taswira ya mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
WAZIRI MAVUNDE ATOA MAAGIZO MATANO KWA MENEJIMENTI YA TUME YA MADINI
habari▪️Asisitiza kuzingatiwa kwa sheria ya Madini
▪️Ataka ofisi za Madini kusimamia haki katika usuluhishi wa migogoro
▪️Maafisa Madini watakiwa kuongeza ubunifu katika utekelezaji majukumu
▪️Makusanyo ya maduhuli yafikia asilimia 86.53_
▪️Apongeza utulivu Sekta ya Madini
WAZIRI wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde (MB) ametoa maelekezo matano kwa Menejimenti ya Tume ya Madini hasa Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuzingatia na kusimamia sheria katika utekelezaji wa majukumu yao na kufikiri nje ya boksi ili kuwa na kitu cha ziada katika kuendeleza Sekta ya Madini.
Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Aprili 30, 2025 jijini Dodoma kwenye ufunguzi wa kikao cha Menejimenti ya Tume ya Madini ambapo amewataka watendaji kuwa wabunifu katika maeneo yao, washirikiane, mkoa mmoja na mkoa mwingine pamoja na kushauriana.
“Kwenye Sekta ya Madini ukiweka sheria pembeni utaivuruga sekta, kuna wakati matumizi ya busara huwa yanahitajika lakini sheria kwanza, kaisimamieni, kesho keshokutwa mtu atakuuliza jambo lingine lolote dhamira yako ilikuwa nini na sheria inasema nini, kasimamie sheria kwanza na kama kuna maelekezo tofauti yasitokane na wewe, wewe katimize wajibu wako wa kusimamia sheria ni muhimu sana,”amesema Waziri Mavunde.
Agizo la pili ambalo amelitoa Mheshimiwa Mavunde ni kutaka ubunifu na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
“Nataka mkawe wabunifu, tumenunua magari 101 mengine yanakuja pikipiki 140 Rais Daktari Samia Suluhu Hassan ametupatia nyenzo, nataka mfikiri nje ya boksi nini ufanye kwenye eneo lako ili sekta iweze kushamiri zaidi, isiwe ‘business as usual’ tunatamani kuona kila mtu katika eneo lake anajitahidi,”amesema.
Katika hatua nyingine Mheshimiwa Mavunde amewapongeza Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kwa ukusanyaji wa maduhuli na kuwataka kutorudi nyuma na kuhakikisha kila mmoja anavuka lengo alilopangiwa na kuongeza kuwa,
“Mjitahidi kutafuta njia za kuongeza makusanyo pasipo kuleta athari kwa watu mnaowasimamia. Zipo njia nyingi za kufanya simamieni hilo, sisi tunaingiza fedha nyingi sana katika mfuko mkuu wa Serikali, miradi inayokuja mikubwa naamini tutafanya vizuri zaidi.
Katika agizo la nne la uadilifu Waziri Mavunde ameeleza kuwa hivi karibuni Sekta ya Madini imekuwa na utulivu pasipo kuwepo na malalamiko yoyote na kuwataka Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuendelea kutenda haki pasipo kuonea wadau wa madini na kutatua migororo na changamoto zinazowakumba wadau wa madini.
![]() |
Amewasisitiza Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuhakikisha wanatatua migogoro kwa kufuata haki ili kujenga imani na wachimbaji wa madini na kuendelea kutoa elimu kuhusu Sheria na Kanuni za Madini ili kupunguza migogoro kabisa.
Akitoa agizo la Tano Mheshimiwa Mavunde amesema kuwa ili kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini, imeundwa kamati maalum ya kuwajengea uwezo watanzania kushiriki kikamilifu katika Sekta ya Madini ili baadaye wawe wachimbaji wakubwa wa madini na kuelekeza Watendaji wa Tume ya Madini kutoa ushirikiano kwa kamati hiyo.
“Wanapokuwepo wachimbaji wakubwa ambao ni wazawa faida lukuki zinapatikana ikiwa ni pamoja na ajira, mapato na ongezeko la manunuzi ya bidhaa na huduma za ndani ya nchi,” amesema Waziri Mavunde.
Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuhamasisha uwekezaji katika ujenzi wa viwanda vya uongezaji thamani madini nchini ambapo mpaka sasa wawekezaji wengi wamejitokeza kwenye ujenzi wa viwanda vya uongezaji thamani katika mikoa ya kimadini ya Chunya, Dodoma, Dar es Salaam, Pwani, Kilimanjaro, Rukwa na Lindi.
Amesema kutokana na utendaji mzuri wa Sekta ya Madini hasa mchango wake kwenye Pato la Taifa kufikia asilimia 10.1 nchi ya Kenya kupitia Waziri wa Madini na Uchumi wa Bluu, Mheshimiwa Ali Hassan Joho wameomba kuja kujifunza nchini Tanzania.
Aidha, amewataka wachimbaji wa madini waliopewa leseni kuzifanyia kazi na kwa ambao hawajazifanyia kazi hatua mbalimbali za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuandikiwa hati za makosa na kufutwa kwa mujibu wa sheria.
![]() |
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba akizungumza katika mkutano huo amewataka Viongozi wa Tume ya Madini kuendelea kuimarisha upendo sambamba na kushirikiana ili Sekta ya Madini iendelee kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa.
Naye Kamishna wa Tume ya Madini, Mhandisi Theonestina Mwasha akielezea hali ya makusanyo ya maduhuli katika Tume ya Madini amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 753.8 sawa na asilimia 85.45 ya lengo kilikusanywa.
Ameongeza kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025 kuanzia mwezi Julai hadi Aprili 29, 2025 Tume ya Madini imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi Bulioni 862.64 ambacho ni sawa na asilimia 86.53 ya lengo la Shilingi Trilioni Moja.
“Tunaamini kiasi kilichobaki tutakikamilisha ifikapo Juni, 30 mwaka huu kwa kuongeza nguvu na ubunifu kwenye ukusanyaji wa maduhuli na udhibiti wa mianya ya upotevu wa mapato,” amesisitiza Kamishna Mwasha.
WATANZANIA WATAKIWA KUENZI MUUNGANO
habariNa Paskal Mbunga, Tanga.