WATANZANIA WATAKIWA KUENZI MUUNGANO

April 29, 2025



Na Paskal Mbunga, Tanga.


WATANZANIA wametakiwa kuuenzi Muungano wa Tanzania kwa sababu ni tunu kubwa tuliyoachiwa na wazee wetu waasisi wa Muungano huo. hayati Mwalimu Julius Nyerere na hayati Mzee Amri Abeid Karume wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

AÄ·izungumza na hadhara ya wakazi wa Jiji la Tanga Jumamosi hii ya kuadhimisha mwaka wa 61 wa kuzaliwa mwungano huo , Spika wa Bunge la Baraza la Mapinduzi Zanzibar,  Zubeir Maulid, alisema kwamba mapinduzi hayo yameleta mafanikio makubwa.

Alitaja mafanikio yaliyoletwa na Muungano huo ni pamoja na uwepo wa Rais Samia Hassan madarakani kwani bila Muungano, Mheshimiwa Samia asingeipata nafasi hiyo kutokana na kigezo cha uraia wake wa Zanzibar.

Alisema kwamba kuungana kwa nchi hizo mbili kumeimarisha ulinzi na usalama katika mipaka yetu ikiwa ni pamoja na ya baharini na nchi kavu.

Akisisitiza umuhimu wa Muungano huo kwa Watanzania, Spika Zubeir alisema uchumi wa nchi mbili hizi umepaa kutokana na kuongezeka kwa biashara kati ya nchi hizo mbili.

Kiongozi huyo kutoka Zanzibar aliwachekesha wananchi waliohudhuria hafla hiyo pale aliposema kwamba matunda ya Muungano ni mengi.   

"Sasa hivi ndoa zimeongezeka sana kati ya  watu wanaooana kutoka Zanzibar na wale kutoka Tanzania Bara".

Hata hivyo, Mheshimiwa Maulid aliwahimiza Watanzania kudumisha amani na kuhakikisha kuwa kila mwenye sifa ya kupiga kùra anahakikisha anatumia haki yake hiyo ifikapo mwezi Oktoba, 2025.

Awali akimkaribisha Mgeni huyo rasmi,  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani alisema kuwa Mkoa wa Tanga uko mbele katika kuitikia wito wa kujiandikisha kupiga kura kwani hadi sasa  Mkoa wa Tanga unaongoza kitaifa kwa kuandisha katika daftari la wapiga kura ambapo hadi sasa waliojiandisha ni karibu asilimia mia moja na sitini.

Naye Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huu, Mhe. Rajabu Abrahamani alimhakikishia Spika Zubeir kwamba kwa mapenzi makubwa waliyomwonyesha Rais Samia wakati wa ziara yake iliyofana sana mkoani hapa mwezi uliopita, ana uhakika kwamba Mkoa huu utaongoza katika kura za kumpigia Rais Samia katika Uchaguzi Mkuu ujao, Oktoba, 2025.

(MWISHO)


Share this

Related Posts

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng