Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

WANANCHI NJOMBE WAIOMBA TANESCO, REA KUONGEZA KASI YA KUWAUNGANISHIA UMEME

March 18, 2025 Add Comment

Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Melela Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Mathayo Davidi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtwango mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi, 2025.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Khatib Kazungu akifafanua jambo kwa wananchi wa Kijiji cha Lwangu Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.

 

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wakala wa Nishati Vijijini(REA), Mhandisi Jones Olotu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lupende Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.



 Hamasa ya kuunganishiwa umeme yatokana na kasi ya maendeleo katika sehemu zenye huduma ya umeme



Kapinga asema ifikapo 2030 Wananchi wote watakuwa wamefikiwa na huduma ya umeme



NJOMBE



Wananchi wa Mkoa wa Njombe ambao bado hawajafikiwa na huduma ya umeme wameiomba Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza kasi ya kuwaunganishia umeme katika kaya zao ili waweze kuutumia kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.



Hayo yameelezwa kupitia Viongozi wa Vijiji vya Melela, Mtwango, Lwangu, Lupende na Melela wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini iliyolenga kukagua maendeleo ya mradi wa usambazaji umeme vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.



Viongozi hao wamesema wananchi wameingia hamasa zaidi ya kuunganishiwa umeme baada ya kuona maendeleo yanazidi kuimarika katika baadhi ya Kaya ambazo tayari zimeunganishiwa umeme.



Aidha, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ambayo imetoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ukiwemo umeme katika maeneo yao ambapo kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakiona kasi kubwa ya maendeleo.



Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amewatoa hofu wananchi hao kwa kuwaeleza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inafikisha umeme kwa wananchi wote ifikapo 2030.



Ameeleza kuwa maendeleo katika maeneo yote hupelekwa kwa hatua kama ilivyo kwa miradi ya umeme lakini lengo la Serikali ni wananchi wote wafikiwe na huduma.



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mathayo David amewasisitiza wananchi kuendelea kutandaza nyaya katika nyumba zao ili miradi ya umeme uiakapowafikia waunganishwe kwa haraka.



Ameeleza kuwa, wananchi ambao hawahitaji kusuka nyaya wafike katika ofisi za TANESCO Ili wapatiwe kifaa cha umeme tayari( UMETA) kwa gharama ya Shilingi elfu 27,000 tu.

WANANCHI NJOMBE WAIOMBA TANESCO, REA KUONGEZA KASI YA KUWAUNGANISHIA UMEME

March 18, 2025 Add Comment

 

Wananchi wa Mkoa wa Njombe ambao bado hawajafikiwa na huduma ya umeme wameiomba Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza kasi ya  kuwaunganishia umeme katika kaya zao ili waweze kuutumia kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hayo yameelezwa kupitia Viongozi wa Vijiji  vya Melela, Mtwango, Lwangu, Lupende na Melela wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini iliyolenga kukagua maendeleo ya  mradi wa usambazaji umeme vijijini katika vijiji vya Mkoa wa  Njombe tarehe 18 Machi 2025.

Viongozi hao wamesema wananchi wameingia hamasa zaidi ya kuunganishiwa umeme baada ya kuona maendeleo yanazidi kuimarika katika baadhi ya Kaya ambazo tayari zimeunganishiwa umeme.

Aidha, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ambayo  imetoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ukiwemo umeme katika maeneo yao ambapo kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakiona kasi kubwa ya maendeleo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amewatoa hofu wananchi hao kwa kuwaeleza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inafikisha umeme kwa wananchi wote ifikapo 2030.

Ameeleza  kuwa maendeleo katika maeneo yote hupelekwa kwa hatua kama ilivyo kwa miradi ya umeme lakini lengo la Serikali ni wananchi wote wafikiwe na huduma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mathayo David amewasisitiza wananchi  kuendelea kutandaza nyaya katika nyumba zao ili miradi ya umeme uiakapowafikia waunganishwe kwa haraka.

Ameeleza kuwa,  wananchi ambao hawahitaji kusuka nyaya wafike katika ofisi za TANESCO Ili wapatiwe kifaa cha umeme tayari( UMETA) kwa gharama ya Shilingi elfu 27,000 tu.

WAZIRI MAVUNDE AGAWA MITUNGI YA GESI KWA MAMALISHE ZAHANATI NA HOSPITALI JIJINI DODOMA

March 18, 2025 Add Comment

 


📌 *Ni sehenu ya utekekezaji wa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia*


Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde leo amegawa  Mitungi ya Gesi kwa Mamalishe, Zahanati na Hospitali Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya utekelezqji wa Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.



Kutoka Wizara ya Nishati  tukio lilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, Bw. Ngeleja Mgejwa.

FAMILIA YA MZEE KING MAJUTO YATOA MSAADA WA FUTARI KWA WATOTO YATIMA TANGA

March 18, 2025 Add Comment

>Yamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kuenzi mchango wa Mzee wao.

Na Oscar Assenga, TANGA

FAMILIA ya Marehemu Mzee King Majuto leo wametoa msaada wa futari katika kituo cha kulea Watoto Yatima cha Goodwill Foundation kilichopo mkoani Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kuisaidi Jamii.

Hatua ya msaada huo ni sehemu ya familia hiyo kurudisha kwa jamii baada ya kupokea fedha taslimu kutoka kwa Rais Milioni 30 ikiwa ni kutambua mchango wa mzee wao katika Tasnia ya Filamu hapa nchini.

Akizungumza mara baada ya kugawa msaada huo Mke wa Marehemu King Majuto,Asha Mbwana Yusuf  alisema wamekwenda kukabidhi sadaka kwa watoto yatima wanaolelewa katika kituo hicho ikiwa ni kuwapunguzia makali ya maisha.

“Tumeona kwenye mwezi mtukufu wa ramadhani mara nyingi katika mwezi huo heri nyingi unazozifanya mwenyezi Mungu anazipokea kwa kushirikiana na Familia tumeona tulifanyie hilo kwa pamoja kuwafikia watoto yatima”Alisema

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Wasanii wa Filamu Mkoa wa Tanga Mohamed Amri Majuto alisema waliamua kufanya hilo kutokana na kwamba huo ni mwezi mtukufu wa ramadhani na kumuenzi baba yao Mzee Amri Athumani Amri Maarufu King Majuto kwa kutoa sadaka hiyo kwa watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu.

“Hii itakuwa ni furaha kwa mzee alipo na sisi kama familia tunajisikia faraja na mioyo yao imekuwa misafi na haya mambo tumekuwa tukilifanya kila wakati na hata mwezi Agosti kila mwaka tumekuwa tukilifanya kumbumbuka mzee wetu kule kwenye malazo yake”Alisema Mohamed Amri Majuto ambaye pia ni Mtoto wa Mzee Majuto.

Awali akizungumza mtoto mwengine wa Mzee Majuto Othumani Amri alisema lengo kubwa ni kutoa shukrani za dhati Rais Samia Suluhu kuwakabidhi fedha taslimu milioni 30 nao wakaona wafanye suala la kumuenzi mzee kutoa sadaka kwenye kituo cha Watoto Yatima.

“Tunamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kumuenzi mzee wetu pamoja na kutukabidhi kiasi cha Milioni 30 na sisi wakaamua kuenzi mzee wao kwa kutoa sadaka kwenye kituo cha watoto yatima hivyo wanamshukuru kwa kumuenzi mzee wao”Alisema

Awali akizungumza ni Katibu wa Taasisi ya Nasimama na Mama Popote Alipo Raphael Kiango alisema wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu na wameona ni matunda ya moja kwa moja yanayotokana na Serikali ya awamu ya sita kwa kuthamini mchango wa wasanii ambao hawapo nao kwenye ulimwengu wa sasa.

Alisema lakini wameamua kumpa tunzo ya heshima na kumpatia kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya familia na hivyo kuleta chachu hamasa kwa wasanii jambo ambalo limepelekea familia hiyo kuamua kutoa sadaka.

“ Tunaishukuru Serikali kwa kumpatia tuzo ya heshima Mzee Wetu King Majuto na kutoa kiasi cha Fedha Milioni 30 hivyo kwetu sisi imekuwa ni faraja kubwa kuona namna jina lake linaishi na tunampongeza Rais Dkt Samia Suluhu ,Wizara ya Habari ,Utamaduni Sanaa na Michezo kuwathimini wasanii hata wale ambao wametangulia mbele za haki”Alisema

Hata hivyo kwa upande wake Mkurugenzi wa Goodwill foundation Sayyed Muhdhar alisema lengo la kuanzishwa taasisi hiyo ni kuisaidia jamiii ikilenga yatima, wazee wasiojiweza na wahitaji huku wakiishukuru familia ya Marehemu Mzee King Majuto kwa kuweza kumfanya mzee majuto kuendelea kuishi.

Alisema kwamba ujio wao umekuwa mzuri kutokana na kuendelea kuenzi aliyokuwa akiyafanya mzee wao kwa kujitolea ikiwemo kuipongeza familia yao kwa kuendelea kumuenzi kumfanya aendelee kuishi.

Mwisho.

TANGA UWASA KUBORESHA UWEZO WA UZALISHAJI MAJI KUFIKIA LITA MILIONI 60

March 17, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) imeweka bayana mpango mkakati wao wa kuboresha uwezo wa uzalishaji wa maji kutoka Lita Milioni 45 mpaka kufikia Lita Milioni 60 pamoja na kuongeza mtandao wa bomba la usambazaji wa maji kwa umbali wa kilomita 60

Mpango huo uliwekwa bayana leo na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Alawi Ahmadi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya wiki ya maji iliyoanza Machi 16 hadi Machi 22, 2025 yenye kauli mbiu “Uhifadhi wa uoto wa asili kwa uhakika wa Maji”

Alisema kwamba lengo la mipango hiyo ni kuhakikisha huduma inafika kwa wakazi wote pamoja na utekelezajii wa miradi mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu kuanzia eneo la Bwawani,Mtambo wa kutibu maji pamoja na kuendeleza mtandao wa usambazaji maji katika maeneo mbalimbali .

“Tutaboresha uwezo wa kuzalisha maji kwa asilimia 25 ukilinganisha na mahitaji kwa sasa tunaweza kuzalisha maji lita milioni 45 tunataka kuzalisha maji lita milioni 60 kutakuwa na ongezeko la maji lita milioni 15 kwenye uwezo uliopo wa mtambo wetu”Alisema

Aidha alisema kwamba wataongeza pia mtandao wa bomba la usambazaji maji kwa kilomita 60 sasa hivi wana urefu wa kilomita 862 lakini wataongeza kilimota 60 ili kufikia watu wote waliopo kwenye eneo lao lka huduma,

Alisema kwamba mradi huo ulianza tokea mwezi Julai mwaka jana na unatarajia kuisha Desemba mwaka huu ambapao kwa sasa umefikia asilimia 15 kwa maana vifaa vyote vinayotakiwa kutekeleza mradi huo vimewasili eneo la mradi na wakandarasi wamekwisha kuanza kazi kwa maeneo mbalimbali.

“Mradi huu vifaa vyote vinavyotakiwa vimewasili na gharama za mradi huo ni Sh.Bilioni 53.12 ambazo walizipata kwa kuuza hati fungani na kwa sasa utoaji huduma umefikia asilimia 93 ya wakazi wa Jiji ya Tanga, Muheza na Pangani”Alisema

Alisema kupitia kauli mbiu hiyo Tanga Uwasa inapanga kufanya tathimini na kuweka vipaumbele kwenye mambo mbalimbali ikiwemo jitahida zinazofanyika na matokeo ya uhifadhi wa mazingira ili kufanikisha kutunza vyanzo vya maji ili viweze kuwa endelevu.

“Lakini kupunguza athari za uchafuzi wa vyanzo vya maji ili kupunguza athari zake kwa watumiaji na kupunguza gharama za kuyasafisha pamoja na utekelezaji wa miradi ya kuboresha hali ya huduma kwa upande wa maji safi na taka”Alisema

Alisema pia kuendelea na utatuzi wa kero za huduma zinazowapata wananchi kwa sasa katika maeneo mbalimbali ya huduma pamoja na kutoa elimu kwa wateja juu ya huduma kwa kutumia vyombo vya habari, madawati ya huduma kwa wateja.

“Katika wiki ya maadhimisho ya wiki ya maji Tanga Uwasa imejipanga kutoa elimu kwa wateja kuhusu masuala mtambuka ya maji kutumia vyombo vya habari, madawati maalumu ya huduma kwa wateja na kuwatembelea majumbani pamoja na kutoa msahama wa tozo ya kurejesha huduma kwa wateja ambao wamesitishiwa huduma ya maji pamoja na kuruhusiwa kuweka mikataba ya kulipa madeni yao kwa awamu yaani kidogo kidogo”Alisema

Awali akizungumza Kaimu Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Tanga Uwasa Mhandisi Salum Hamis alisema wana mradi mkubwa wa hati fungani ambapo wana maeneo makubwa manne ambayo yatasaidia kumaliza shida ya maji katika Jiji la Tanga na miji ya Muheza na Pangani.

Alisema kwenye huo mradi wanakwenda kuupanua mtambo wa kusukuma maji mabayani kutoka uwezo wa sasa wa kusumua maji kutoka Lita 42,000 kwa siku mpaka kufika 60,000 kwa siku ikiwemo kujenga bomba linguine kubwa kutoka mabayani mpaka kituo chao cha kusafisha maji Mowe lenye kipenyo cha Milimita 600.

“Sasa hivi wana Bombo lenye milimita 600 na wanaongeza la pili na lingine ni kituo cha kusafisha na kutibu maji Mowe kwa sasa kina uwezo wa kusafisha na kutibu maji kwa uwezo wa mita za ujazo 45,000 kwa siku kwenye huo mradi tunakwenda kukiongeza kufikia uwezo wa mita za ujazo 60,000 kwa siku “Alisema